Zaburi 99:1-9

  • Yehova ni Mufalme mutakatifu

    • Amekaa akiwa mufalme juu ya makerubi (1)

    • Mungu mwenye kusamehe na kutoa malipizi (8)

99  Yehova amekuwa Mufalme.+ Acha vikundi vya watu vitetemeke. Anakaa akiwa mufalme juu ya* makerubi.+ Acha dunia itikisike.   Yehova ni mukubwa katika Sayuni, Na iko* juu kuliko vikundi vyote vya watu.+   Acha wasifu jina lako kubwa,+ Kwa maana ni lenye kuogopesha sana na liko takatifu.   Yeye ni mufalme mwenye nguvu ambaye anapenda haki.+ Umefanya mambo manyoofu yakuwe imara kabisa. Umeleta haki na uadilifu*+ katika Yakobo.   Mumutukuze Yehova Mungu wetu+ na kuinama* mbele ya kiti cha miguu yake;+ Yeye ni mutakatifu.+   Musa na Haruni walikuwa kati ya makuhani wake,+ Na Samweli alikuwa kati ya wale wenye walikuwa wanaitia jina lake.+ Walikuwa wanamuita Yehova, Na alikuwa anawajibu.+   Alikuwa anasema nao kutoka katika nguzo ya wingu.+ Walishika vikumbusho vyake na agizo lenye aliwapatia.+   Ee Yehova Mungu wetu, uliwajibu.+ Ulikuwa Mungu mwenye aliwasamehe,+ Lakini uliwapatia azabu* kwa sababu ya matendo yao ya zambi.+   Mumutukuze Yehova Mungu wetu+ Na muiname* mbele ya mulima wake mutakatifu,+ Kwa maana Yehova Mungu wetu ni mutakatifu.+

Maelezo ya Chini

Ao pengine, “katikati ya.”
Ao “eko.”
Angalia Maana ya Maneno.
Ao “kuabudu.”
Tnn., “ulilipiza kisasi juu yao.”
Ao “muabudu.”