Zaburi 36:1-12

  • Upendo mushikamanifu wa Mungu wenye samani

    • Muovu hamuogope Mungu (1)

    • Mungu ni chanzo cha uzima (9)

    • “Kupitia mwangaza wako tunaweza kuona mwangaza” (9)

Kwa kiongozi. Ya Daudi,mutumishi wa Yehova. 36  Kosa linazungumuza na muovu ndani kabisa ya moyo wake;Hakuna kumuogopa Mungu mbele ya macho yake.+  2  Kwa maana anajisifu-sifu sana mbele ya macho yake mwenyeweIli asiweze kutambua kosa lake na kulichukia.+  3  Maneno ya kinywa chake yanaumiza na ni ya udanganyifu;Haonyeshe ufahamu wowote wa kutenda mambo ya muzuri.  4  Anafanya mipango yenye kuumiza hata katika kitanda chake. Anafuata njia yenye haiko ya muzuri;Hakatae mambo ya mubaya.  5  Ee Yehova, upendo wako mushikamanifu unafika mupaka mbinguni,+Uaminifu wako mupaka kwenye mawingu.  6  Haki yako iko kama milima mikubwa;*+Hukumu zako ni kama maji mengi yenye kuenda chini sana.+ Unalinda* mwanadamu na munyama, Ee Yehova.+  7  Upendo wako mushikamanifu ni wenye samani sana, Ee Mungu!+ Katika kivuli cha mabawa yako,wana wa binadamu wanakimbilia.+  8  Wanakunywa na kushiba vitu vyenye kunona vya* nyumba yako,+Na unawanywesha kwenye muto wa vitu vyako vyenye kufurahisha.+  9  Kwako kuko chemchemi ya uzima;+Kupitia mwangaza wako tunaweza kuona mwangaza.+ 10  Endelea kuonyesha upendo wako mushikamanifu kwa wale wenye kukujua,+Na haki yako, kwa wale wenye kuwa wanyoofu katika moyo.+ 11  Usiruhusu muguu wa mwenye majivuno unikanyangeWala mukono wa muovu unifukuze. 12  Wakosaji wameanguka kule;Wamepigwa na kuangushwa chini na hawawezi kusimama.+

Maelezo ya Chini

Tnn., “kama milima ya Mungu.”
Ao “Unaokoa.”
Tnn., “unono wa.”