Zaburi 36:1-12
Kwa kiongozi. Ya Daudi,mutumishi wa Yehova.
36 Kosa linazungumuza na muovu ndani kabisa ya moyo wake;Hakuna kumuogopa Mungu mbele ya macho yake.+
2 Kwa maana anajisifu-sifu sana mbele ya macho yake mwenyeweIli asiweze kutambua kosa lake na kulichukia.+
3 Maneno ya kinywa chake yanaumiza na ni ya udanganyifu;Haonyeshe ufahamu wowote wa kutenda mambo ya muzuri.
4 Anafanya mipango yenye kuumiza hata katika kitanda chake.
Anafuata njia yenye haiko ya muzuri;Hakatae mambo ya mubaya.
5 Ee Yehova, upendo wako mushikamanifu unafika mupaka mbinguni,+Uaminifu wako mupaka kwenye mawingu.
6 Haki yako iko kama milima mikubwa;*+Hukumu zako ni kama maji mengi yenye kuenda chini sana.+
Unalinda* mwanadamu na munyama, Ee Yehova.+
7 Upendo wako mushikamanifu ni wenye samani sana, Ee Mungu!+
Katika kivuli cha mabawa yako,wana wa binadamu wanakimbilia.+
8 Wanakunywa na kushiba vitu vyenye kunona vya* nyumba yako,+Na unawanywesha kwenye muto wa vitu vyako vyenye kufurahisha.+
9 Kwako kuko chemchemi ya uzima;+Kupitia mwangaza wako tunaweza kuona mwangaza.+
10 Endelea kuonyesha upendo wako mushikamanifu kwa wale wenye kukujua,+Na haki yako, kwa wale wenye kuwa wanyoofu katika moyo.+
11 Usiruhusu muguu wa mwenye majivuno unikanyangeWala mukono wa muovu unifukuze.
12 Wakosaji wameanguka kule;Wamepigwa na kuangushwa chini na hawawezi kusimama.+