Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Utangulizi

Biblia Takatifu ni ujumbe wa Mungu wenye uliandikwa kwa ajili ya sisi wote. Tunapaswa kujifunza Biblia hiyo ili tumujue Mutungaji wake. (Yohana 17:3; 2 Timoteo 3:16) Katika kurasa za Biblia, Yehova Mungu anafunua kusudi lake kwa ajili ya wanadamu na kwa ajili ya makao yao, ni kusema, dunia.—Mwanzo 3:15; Ufunuo 21:3, 4.

Hakuna kitabu kingine chenye kinasaidia watu sana katika maisha kama vile Biblia. Biblia inatuchochea tuonyeshe sifa za Yehova, kama vile, upendo, rehema, na huruma. Inatupatia tumaini, na katika njia hiyo inasaidia watu wavumilie hata mateso makali zaidi. Na inaendelea kuonyesha waziwazi mambo ya ulimwengu huu yenye hayapatane na mapenzi makamilifu ya Mungu.—Zaburi 119:105; Waebrania 4:12; 1 Yohana 2:15-17.

Biblia iliandikwa kwanza katika Kiebrania, Kiaramu, na Kigiriki; imetafsiriwa ikiwa nzima ao ikiwa sehemu, katika luga karibu elfu tatu (3000). Biblia ndicho kitabu chenye kimetafsiriwa na kugawanywa sana katika historia. Hilo halipaswe kutushangaza. Unabii mumoja wa Biblia unasema hivi: “Hii habari njema ya Ufalme [ujumbe wa maana sana wenye kuwa katika Biblia] itahubiriwa katika dunia yote yenye kuikaliwa na watu ili kuwa ushahidi kwa mataifa yote, na kisha ule mwisho utakuja.”—Matayo 24:14.

Kwa sababu tunatambua kwamba ujumbe wa Biblia ni wa maana, tumeamua kurekebisha maandishi haya tukiwa na heshima kubwa kwa ajili ya mambo yenye kupatikana katika Biblia. Tunajisikia kuwa na daraka nzito la kutafsiri ujumbe wake bila makosa. Chapa hii yenye kurekebishwa imejenga musingi juu ya chapa za Kiingereza zenye zilitangulia za New World Translation of the Holy Scriptures, Biblia yenye ilitolewa kwa mara ya kwanza kumepita miaka zaidi ya makumi sita (60). Lakini, luga ya Kiingereza imebadilika katika miaka makumi tano (50) yenye imepita. Badiliko hilo lilichochea washiriki wa sasa wa Halmashauri ya Kutafsiri Biblia ya Ulimwengu Mupya waanze kazi hii ya kuirekebisha. Kusudi letu limekuwa kutoa tafsiri yenye inafuata kwa uaminifu maandishi ya kwanza na pia yenye kuwa wazi na mwepesi kusoma. Marekebisho fulani ya luga yenye yalifanywa katika tafsiri hii yanazungumuziwa katika Nyongeza “Kanuni za Kutafsiri Biblia,” “Mambo ya Maana ya Tafsiri Hii Yenye Ilirekebishwa,” na “Namna Biblia Ilitufikia.”

Wale wenye wanamupenda Yehova Mungu na kumuabudu wanataka kuwa na tafsiri yenye haina makosa, yenye kueleweka ya Neno la Mungu. (1 Timoteo 2:4) Ndiyo maana tumetokeza Biblia hii yenye kurekebishwa katika Swahili (Congo), tukiwa na nia ya kuitafsiri katika luga nyingi kadiri inawezekana. Tunatumaini na kusali kwamba wewe, musomaji mupendwa, utaona tafsiri hii ya Maandiko Matakatifu kuwa yenye faida wakati unajikaza ‘kumutafuta Mungu . . . na kwa kweli umupate.’—Matendo 17:27.

New World Bible Translation Committee

Mwezi wa 8, 2013