Zaburi 15:1-5

  • Ni nani anaweza kuwa mugeni katika hema ya Yehova?

    • Anasema kweli katika moyo wake (2)

    • Hasingizie (3)

    • Anatimiza ahadi hata wakati inaleta matatizo (4)

Muziki wa Daudi. 15  Ee Yehova, ni nani anaweza kuwa mugeni katika hema yako? Ni nani anaweza kukaa katika mulima wako mutakatifu?+  2  Ule mwenye anatembea bila kosa,*+Mwenye anazoea kufanya mambo yenye kuwa sawa+Na kusema kweli katika moyo wake.+  3  Hasingizie kwa ulimi wake,+Hamutendee jirani yake jambo lolote la mubaya,+Naye hawaharibishie marafiki wake sifa.*+  4  Anamukataa mutu yeyote mwenye kuzarauliwa,+Lakini anaheshimia wale wenye kumuogopa Yehova. Havunje ahadi yake,* hata wakati inamuletea matatizo.+  5  Hakopeshe feza zake kwa ajili ya faida,+Na hakubali rushwa* ili kumutesa mwenye hana kosa.+ Mutu yeyote mwenye kufanya mambo hayo hatatikiswa* hata kidogo.+

Maelezo ya Chini

Ao “kwa uaminifu-mushikamanifu.”
Ao “hawapatishe haya marafiki wake.”
Tnn., “kiapo chake.”
Ao “kata-midomo.”
Ao “hatayumba-yumba.”