Zaburi 15:1-5
Muziki wa Daudi.
15 Ee Yehova, ni nani anaweza kuwa mugeni katika hema yako?
Ni nani anaweza kukaa katika mulima wako mutakatifu?+
2 Ule mwenye anatembea bila kosa,*+Mwenye anazoea kufanya mambo yenye kuwa sawa+Na kusema kweli katika moyo wake.+
3 Hasingizie kwa ulimi wake,+Hamutendee jirani yake jambo lolote la mubaya,+Naye hawaharibishie marafiki wake sifa.*+
4 Anamukataa mutu yeyote mwenye kuzarauliwa,+Lakini anaheshimia wale wenye kumuogopa Yehova.
Havunje ahadi yake,* hata wakati inamuletea matatizo.+
5 Hakopeshe feza zake kwa ajili ya faida,+Na hakubali rushwa* ili kumutesa mwenye hana kosa.+
Mutu yeyote mwenye kufanya mambo hayo hatatikiswa* hata kidogo.+

