Zaburi 84:1-12

  • Kutamani sana tabenakulo kubwa ya Mungu

    • Mulawi anatamani kuwa kama ndege (3)

    • “Siku moja katika viwanja vyako” (10)

    • “Mungu ni jua na ngao” (11)

Kwa kiongozi; juu ya Gititi.* Ya wana wa Kora.+ Muziki. 84  Tabenakulo yako kubwa ni yenye kupendeza sana,*+Ee Yehova wa majeshi!  2  Nafsi yangu yote inatamani sana,Ndiyo, ninazimia kwa kutamani,Viwanja vya Yehova.+ Moyo wangu na mwili wangu vinamupigia Mungu mwenye kuishi vigelegele vya shangwe.  3  Hata ndege anapata makao kuleNa mbaruwayu anajipatia chicha,*Kwenye anatunza vitoto vyakeKaribu na mazabahu yako kubwa, Ee Yehova wa majeshi,Mufalme wangu na Mungu wangu!  4  Wenye furaha ni wale wenye wanakaa katika nyumba yako!+ Wanaendelea kukusifu.+ (Sela)  5  Wenye furaha ni watu wenye wanapata nguvu kutoka kwako,+Wenye mioyo yao imekazwa juu ya barabara kubwa.  6  Wakati wanapita katika Bonde la Mibaka,*Wanalifanya kuwa mahali kwenye chemchemi;Na mvua ya kwanza inalivalisha* baraka.  7  Wataendelea kutembea kutoka nguvu mupaka nguvu zaidi;+Kila mumoja wao anaonekana mbele ya Mungu kule Sayuni.  8  Ee Yehova Mungu wa majeshi, sikia sala yangu;Sikiliza, Ee Mungu wa Yakobo. (Sela)  9  Angalia, ngao yetu+ na Mungu wetu,*Angalia uso wa mutiwa-mafuta wako.+ 10  Kwa maana siku moja katika viwanja vyako inapita siku elfu moja (1 000) mahali pengine popote!+ Ninachagua kusimama kwenye muingilio wa* nyumba ya Mungu wanguKuliko kukaa katika mahema ya uovu. 11  Kwa maana Yehova Mungu ni jua+ na ngao;+Anatoa wema na utukufu. Yehova hatawaima jambo lolote la muzuriWale wenye kutembea kwa uaminifu-mushikamanifu.+ 12  Ee Yehova wa majeshi,Mwenye furaha ni mutu mwenye anakutegemea.+

Maelezo ya Chini

Ao “yenye kupendwa sana.”
Ao “nyumba ya ndege; kiota.”
Ao “bonde la miti midogo-midogo ya mibaka.”
Ao pengine, “Na mufundishaji anajifunika mwenyewe.”
Ao pengine, “Angalia ngao yetu, Ee Mungu.”
Ao “kizingiti cha.”