Zaburi 84:1-12
Kwa kiongozi; juu ya Gititi.* Ya wana wa Kora.+ Muziki.
84 Tabenakulo yako kubwa ni yenye kupendeza sana,*+Ee Yehova wa majeshi!
2 Nafsi yangu yote inatamani sana,Ndiyo, ninazimia kwa kutamani,Viwanja vya Yehova.+
Moyo wangu na mwili wangu vinamupigia Mungu mwenye kuishi vigelegele vya shangwe.
3 Hata ndege anapata makao kuleNa mbaruwayu anajipatia chicha,*Kwenye anatunza vitoto vyakeKaribu na mazabahu yako kubwa, Ee Yehova wa majeshi,Mufalme wangu na Mungu wangu!
4 Wenye furaha ni wale wenye wanakaa katika nyumba yako!+
Wanaendelea kukusifu.+ (Sela)
5 Wenye furaha ni watu wenye wanapata nguvu kutoka kwako,+Wenye mioyo yao imekazwa juu ya barabara kubwa.
6 Wakati wanapita katika Bonde la Mibaka,*Wanalifanya kuwa mahali kwenye chemchemi;Na mvua ya kwanza inalivalisha* baraka.
7 Wataendelea kutembea kutoka nguvu mupaka nguvu zaidi;+Kila mumoja wao anaonekana mbele ya Mungu kule Sayuni.
8 Ee Yehova Mungu wa majeshi, sikia sala yangu;Sikiliza, Ee Mungu wa Yakobo. (Sela)
9 Angalia, ngao yetu+ na Mungu wetu,*Angalia uso wa mutiwa-mafuta wako.+
10 Kwa maana siku moja katika viwanja vyako inapita siku elfu moja (1 000) mahali pengine popote!+
Ninachagua kusimama kwenye muingilio wa* nyumba ya Mungu wanguKuliko kukaa katika mahema ya uovu.
11 Kwa maana Yehova Mungu ni jua+ na ngao;+Anatoa wema na utukufu.
Yehova hatawaima jambo lolote la muzuriWale wenye kutembea kwa uaminifu-mushikamanifu.+
12 Ee Yehova wa majeshi,Mwenye furaha ni mutu mwenye anakutegemea.+

