Zaburi 135:1-21
135 Mumusifu Yah!*
Musifu jina la Yehova;Mutoe sifa, ninyi watumishi wa Yehova,+
2 Ninyi wenye kusimama katika nyumba ya Yehova,Katika viwanja vya nyumba ya Mungu wetu.+
3 Mumusifu Yah, kwa maana Yehova ni mwema.+
Muimbie jina lake sifa,* kwa maana ni lenye kupendeza.
4 Kwa maana Yah amemuchagua Yakobo kwa ajili yake mwenyewe,Israeli kuwa mali yake ya pekee.*+
5 Kwa maana ninajua muzuri kwamba Yehova ni mukubwa;Bwana wetu ni mukubwa kuliko miungu mingine yote.+
6 Yehova anafanya kila kitu chenye anapenda kufanya+Katika mbingu na juu ya dunia, katika bahari na katika sehemu za chini kabisa.
7 Anafanya mawingu yapande* kutoka kwenye miisho ya dunia;Anatokeza umeme wa radi kwa ajili ya* mvua;Analeta upepo kutoka katika madepo yake.+
8 Alipiga na kuua muzaliwa wa kwanza wa Misri,Mwanadamu na munyama pia.+
9 Alituma alama na miujiza kati yako, Ee Misri,+Juu ya Farao na watumishi wake wote.+
10 Alipiga na kuua mataifa mengi+Na kuua wafalme wenye nguvu+
11 —Sihoni mufalme wa Waamori,+Ogu mufalme wa Bashani,+Na falme zote za Kanaani.
12 Alitoa inchi yao kuwa uriti,Uriti kwa watu wake Israeli.+
13 Ee Yehova, jina lako linadumu milele.
Ee Yehova, sifa yako inadumu* katika vizazi vyote.+
14 Kwa maana Yehova atatetea* watu wake,+Na atasikilia huruma* watumishi wake.+
15 Sanamu za mataifa ni feza na zahabu,Kazi ya mikono ya mwanadamu.+
16 Ziko na kinywa, lakini haziwezi kusema;+Ziko na macho, lakini haziwezi kuona;
17 Ziko na masikio, lakini haziwezi kusikia.
Hakuna pumuzi katika kinywa chao.+
18 Watu wenye kuzitengeneza watakuwa kama vile sanamu hizo,+Na wale wote wenye kuzitegemea.+
19 Ee nyumba ya Israeli, mumusifu Yehova.
Ee nyumba ya Haruni, mumusifu Yehova.
20 Ee nyumba ya Lawi, mumusifu Yehova.+
Ninyi wenye kumuogopa Yehova, mumusifu Yehova.
21 Yehova asifiwe kutoka Sayuni,+Yeye mwenye kukaa Yerusalemu.+
Mumusifu Yah!+
Maelezo ya Chini
^ Ao “Haleluya!” “Yah” ni kifupi cha jina Yehova.
^ Ao “Mupigie jina lake muziki.”
^ Ao “mali yake yenye anapendezwa nayo sana.”
^ Ao pengine, “Anatengeneza milango kwa ajili ya.”
^ Ao “mivuke ipande.”
^ Ao “jina lako linadumu.” Tnn., “ukumbusho wako unadumu.”
^ Ao “atatetea mashitaka ya.”
^ Ao “atasikitikia.”

