Zaburi 125:1-5

  • Yehova analinda watu wake

    • “Kama vile milima inazunguka Yerusalemu” (2)

    • “Amani ikuwe juu ya Israeli” (5)

Wimbo wa Safari za Kupanda. 125  Wale wenye kumutegemea Yehova+Wako kama Mulima Sayuni, wenye hauwezi kutikiswaLakini unadumu milele.+  2  Kama vile milima inazunguka Yerusalemu,+Ni vile Yehova anazunguka watu wake+Kuanzia sasa na milele.  3  Fimbo ya ufalme ya uovu haitadumu katika inchi yenye iligawiwa wenye haki,+Ili wenye haki wasianze kufanya* makosa.+  4  Ee Yehova, tendea mema wale wenye kuwa wema,+Wenye kuwa wanyoofu katika moyo.+  5  Lakini wale wenye kugeuka pembeni na kufuata njia zao zenye kupotoka,Yehova atawaondoa pamoja na wakosaji.+ Amani ikuwe juu ya Israeli.

Maelezo ya Chini

Ao “wasielekeze mikono yao kwenye.”