Zaburi 21:1-13
Kwa kiongozi. Muziki wa Daudi.
21 Ee Yehova, mufalme anashangilia katika nguvu zako;+Anashangilia sana kabisa katika matendo yako ya wokovu!+
2 Umetimiza tamaa ya moyo wake,+Na haujamuima ombi la midomo yake. (Sela)
3 Kwa maana unakutana naye ukiwa na baraka nyingi;Unatia taji la zahabu safi* kwenye kichwa chake.+
4 Alikuomba uzima, na ukamupatia uzima huo,+Maisha ya murefu,* milele na milele.
5 Matendo yako ya wokovu yanamuletea utukufu mukubwa.+
Unamupatia heshima na uzuri.
6 Unamufanya akuwe mwenye kubarikiwa milele;+Unamufanya afurahi kwa shangwe ya kuwa mbele yako.*+
7 Kwa maana mufalme anamutegemea Yehova;+Kwa sababu ya upendo mushikamanifu wa Mwenye Kuwa Juu Zaidi, hatatikiswa* hata kidogo.+
8 Mukono wako utapata maadui wako wote;Mukono wako wa kuume utapata wale wenye kukuchukia.
9 Utawafanya wakuwe kama tanuru yenye moto kwa wakati wenye uliwekwa wa kuwakazia uangalifu.
Yehova atawameza kwa kasirani yake, na moto utawateketeza.+
10 Utaharibu wazao wao* kutoka katika dunia,Na uzao wao kutoka kati ya wana wa binadamu.
11 Kwa maana walikusudia kukutendea mambo ya mubaya;+Wamefanya mipango mibaya yenye haitakuwa na matokeo ya muzuri.+
12 Kwa maana utawafanya wakimbie+Kwa kuwalenga* kwa upinde wako.*
13 Simama, Ee Yehova, katika nguvu zako.
Tutaimbia uwezo wako sifa.*

