Zaburi 21:1-13

  • Baraka juu ya mufalme mwenye kumutegemea Yehova

    • Mufalme anapewa maisha marefu (4)

    • Maadui wa Mungu watashindwa (8-12)

Kwa kiongozi. Muziki wa Daudi. 21  Ee Yehova, mufalme anashangilia katika nguvu zako;+Anashangilia sana kabisa katika matendo yako ya wokovu!+  2  Umetimiza tamaa ya moyo wake,+Na haujamuima ombi la midomo yake. (Sela)  3  Kwa maana unakutana naye ukiwa na baraka nyingi;Unatia taji la zahabu safi* kwenye kichwa chake.+  4  Alikuomba uzima, na ukamupatia uzima huo,+Maisha ya murefu,* milele na milele.  5  Matendo yako ya wokovu yanamuletea utukufu mukubwa.+ Unamupatia heshima na uzuri.  6  Unamufanya akuwe mwenye kubarikiwa milele;+Unamufanya afurahi kwa shangwe ya kuwa mbele yako.*+  7  Kwa maana mufalme anamutegemea Yehova;+Kwa sababu ya upendo mushikamanifu wa Mwenye Kuwa Juu Zaidi, hatatikiswa* hata kidogo.+  8  Mukono wako utapata maadui wako wote;Mukono wako wa kuume utapata wale wenye kukuchukia.  9  Utawafanya wakuwe kama tanuru yenye moto kwa wakati wenye uliwekwa wa kuwakazia uangalifu. Yehova atawameza kwa kasirani yake, na moto utawateketeza.+ 10  Utaharibu wazao wao* kutoka katika dunia,Na uzao wao kutoka kati ya wana wa binadamu. 11  Kwa maana walikusudia kukutendea mambo ya mubaya;+Wamefanya mipango mibaya yenye haitakuwa na matokeo ya muzuri.+ 12  Kwa maana utawafanya wakimbie+Kwa kuwalenga* kwa upinde wako.* 13  Simama, Ee Yehova, katika nguvu zako. Tutaimbia uwezo wako sifa.*

Maelezo ya Chini

Ao “yenye ilisafishwa.”
Tnn., “Urefu wa siku.”
Tnn., “mbele ya uso wako.”
Ao “hatayumba-yumba.”
Tnn., “matunda yao.”
Tnn., “kulenga nyuso zao.”
Tnn., “kamba zako za upinde.”
Tnn., “Tutaimbia na kupigia muziki uwezo wako.”