Zaburi 91:1-16

  • Ulinzi mahali pa siri pa Mungu

    • Kuokolewa kutoka kwa muwindaji wa ndege (3)

    • Kukimbilia chini ya mabawa ya Mungu (4)

    • Usalama hata kama maelfu wanaanguka (7)

    • Malaika wanaamuriwa kutoa ulinzi (11)

91  Mutu yeyote mwenye kukaa mahali pa siri pa Mwenye Kuwa Juu Zaidi+Ataishi katika kivuli cha Mweza-Yote.+  2  Nitamuambia Yehova: “Wewe ni kimbilio langu na ngome yangu,+Mungu wangu mwenye ninategemea.”+  3  Kwa maana atakuokoa katika mutego wa muwindaji wa ndege,Katika ugonjwa wa kuambukiza wenye kuharibu.  4  Atakufunika kwa manyoya yake,*Na utakimbilia chini ya mabawa yake.+ Uaminifu wake+ utakuwa ngao kubwa+ na ukuta wa ulinzi.*  5  Hautaogopa mambo yenye kuogopesha sana ya usiku,+Wala mushale wenye kuruka muchana,+  6  Wala ugonjwa wa kuambukiza wenye kuwinda kimya-kimya katika giza,Wala uharibifu wenye kuharibu katikati ya muchana.  7  Elfu moja (1 000) wataanguka pembeni yakoNa elfu kumi (10 000) kwenye mukono wako wa kuume,Lakini haitakukaribia wewe.+  8  Utaiona tu kwa macho yakoWakati utajionea azabu* ya waovu.  9  Kwa sababu ulisema: “Yehova ni kimbilio langu,”Umemufanya Mwenye Kuwa Juu Zaidi kuwa makao yako;*+ 10  Hakuna musiba wenye utakufikia,+Na hakuna pigo lenye litakaribia hema yako. 11  Kwa maana ataamuru malaika wake+ kwa ajili yako,Ili wakulinde katika njia zako zote.+ 12  Watakubeba katika mikono yao,+Ili usigonge muguu wako kwenye jiwe.+ 13  Utakanyanga mwana-simba na nyoka-kobra;Utamukanyangia chini simba mwenye manyoya ya murefu kwenye shingo na nyoka mukubwa.+ 14  Mungu alisema: “Kwa sababu ananipenda,* nitamuokoa.+ Nitamulinda kwa sababu anajua* jina langu.+ 15  Ataniitia, na nitamujibu.+ Nitakuwa pamoja naye katika taabu.+ Nitamuokoa na kumutukuza. 16  Nitamushibisha kwa maisha ya murefu,+Na nitamufanya aone matendo yangu ya wokovu.*+

Maelezo ya Chini

Ao “Kupitia manyoya yake ataweka kizuizi ili usifikiwe.”
Ao “boma.”
Tnn., “malipo.”
Ao pengine, “ngome yako; kimbilio lako.”
Tnn., “amejiunga na mimi.”
Ao “anatambua.”
Ao “aone wokovu kutoka kwangu.”