Zaburi 91:1-16
91 Mutu yeyote mwenye kukaa mahali pa siri pa Mwenye Kuwa Juu Zaidi+Ataishi katika kivuli cha Mweza-Yote.+
2 Nitamuambia Yehova: “Wewe ni kimbilio langu na ngome yangu,+Mungu wangu mwenye ninategemea.”+
3 Kwa maana atakuokoa katika mutego wa muwindaji wa ndege,Katika ugonjwa wa kuambukiza wenye kuharibu.
4 Atakufunika kwa manyoya yake,*Na utakimbilia chini ya mabawa yake.+
Uaminifu wake+ utakuwa ngao kubwa+ na ukuta wa ulinzi.*
5 Hautaogopa mambo yenye kuogopesha sana ya usiku,+Wala mushale wenye kuruka muchana,+
6 Wala ugonjwa wa kuambukiza wenye kuwinda kimya-kimya katika giza,Wala uharibifu wenye kuharibu katikati ya muchana.
7 Elfu moja (1 000) wataanguka pembeni yakoNa elfu kumi (10 000) kwenye mukono wako wa kuume,Lakini haitakukaribia wewe.+
8 Utaiona tu kwa macho yakoWakati utajionea azabu* ya waovu.
9 Kwa sababu ulisema: “Yehova ni kimbilio langu,”Umemufanya Mwenye Kuwa Juu Zaidi kuwa makao yako;*+
10 Hakuna musiba wenye utakufikia,+Na hakuna pigo lenye litakaribia hema yako.
11 Kwa maana ataamuru malaika wake+ kwa ajili yako,Ili wakulinde katika njia zako zote.+
12 Watakubeba katika mikono yao,+Ili usigonge muguu wako kwenye jiwe.+
13 Utakanyanga mwana-simba na nyoka-kobra;Utamukanyangia chini simba mwenye manyoya ya murefu kwenye shingo na nyoka mukubwa.+
14 Mungu alisema: “Kwa sababu ananipenda,* nitamuokoa.+
Nitamulinda kwa sababu anajua* jina langu.+
15 Ataniitia, na nitamujibu.+
Nitakuwa pamoja naye katika taabu.+
Nitamuokoa na kumutukuza.
16 Nitamushibisha kwa maisha ya murefu,+Na nitamufanya aone matendo yangu ya wokovu.*+
Maelezo ya Chini
^ Ao “Kupitia manyoya yake ataweka kizuizi ili usifikiwe.”
^ Ao “boma.”
^ Tnn., “malipo.”
^ Ao pengine, “ngome yako; kimbilio lako.”
^ Tnn., “amejiunga na mimi.”
^ Ao “anatambua.”
^ Ao “aone wokovu kutoka kwangu.”