Zaburi 78:1-72
Maskili.* Ya Asafu.+
78 Musikilize sheria yangu,* watu wangu;Mutege sikio lenu kwenye maneno ya kinywa changu.
2 Nitafungua kinywa changu kwa mezali.
Nitaleta maana ya vitendawili vya zamani sana.+
3 Mambo yenye tumesikia na kujua,Yenye baba zetu wametuelezea,+
4 Hatutawaficha wana wao;Tutaelezea kizazi chenye kuja+Matendo ya Yehova yenye kustahili sifa na nguvu zake,+Mambo ya ajabu yenye amefanya.+
5 Alitia kikumbusho katika YakoboNa kuweka sheria katika Israeli;Aliamuru mababu zetuWajulishe watoto wao mambo hayo,+
6 Ili kizazi chenye kitafuata,Watoto wenye hawajazaliwa, wayajue.+
Wao pia wataelezea watoto wao.+
7 Halafu watoto hao watatia tumaini lao katika Mungu.
Hawatasahau kazi za Mungu+Lakini watashika amri zake.+
8 Kisha hawatakuwa kama mababu zao,Kizazi chenye kiko kichwa-nguvu na chenye kuasi,+Kizazi chenye kilikuwa na moyo wenye kuyumba-yumba*+Na chenye hakikukuwa na roho ya uaminifu kwa Mungu.
9 Waefraimu walikuwa wenye kubeba upinde,Lakini walikimbia siku ya vita.
10 Hawakushika agano la Mungu+Na walikataa kutembea katika sheria yake.+
11 Walisahau pia mambo yenye alikuwa amefanya,+Kazi zake za ajabu zenye aliwaonyesha.+
12 Alifanya mambo ya ajabu mbele ya macho ya mababu zao,+Katika inchi ya Misri, eneo la Soani.+
13 Alipasua bahari ili kuwaacha wavuke,Na akafanya maji yasimame kama ukuta wa maji.*+
14 Aliwaongoza kupitia wingu wakati wa muchanaNa usiku wote kupitia mwangaza wa moto.+
15 Alipasua miamba katika jangwa,Akawanywesha maji ya kutosha kama vile yanatoka katika maji yenye kuenda chini sana.+
16 Alifanya mito midogo itoke katika mwambaNa kufanya maji yatiririke chini kama mito.+
17 Lakini waliendelea kumutendea zambiKwa kumuasi katika jangwa ule Mwenye Kuwa Juu Zaidi;+
18 Walishindana na* Mungu katika moyo wao+Kwa kuomba kwa mukazo chakula chenye walitamani.*
19 Kwa hiyo wakasema mubaya juu ya Mungu,Wakisema: “Je, Mungu anaweza kuandaa meza katika jangwa?”+
20 Angalia! Alipiga mwambaNa hivyo maji yakatiririka na mito midogo ikajaa sana.+
“Je, anaweza pia kutupatia mukate,Ao je, anaweza kupatia watu wake nyama?”+
21 Wakati Yehova aliwasikia, akakasirika sana;+Moto+ ukawaka juu ya Yakobo,Na kasirani yake ikawaka juu ya Israeli+
22 Kwa sababu hawakukuwa na imani katika Mungu;+Hawakutegemea uwezo wake wa kuwaokoa.
23 Kwa hiyo akaamuru anga la juu lenye mawingu,Na akafungua milango ya mbingu.
24 Akaendelea kuwanyeshea mana ili wakule;Akawapatia nafaka ya mbinguni.+
25 Wanadamu wakakula mukate wa wenye nguvu;*+Aliwapatia mukate wa kuenea ili kuwashibisha.+
26 Alivumisha upepo wa mashariki katika mbinguNa kwa nguvu zake akafanya upepo wa kusini uvume.+
27 Na akawanyeshea nyama kama mavumbi,Ndege kama muchanga pembeni ya bahari.
28 Aliwaangusha katikati ya kambi yake,Kuzunguka mahema yake pande zote.
29 Na walikula na kula kwa ulafi;Aliwapatia kile walitamani.+
30 Lakini mbele watosheleze kikamili tamaa yao,Wakati chakula kilikuwa kingali katika kinywa chao,
31 Kasirani kali ya Mungu ikawaka juu yao.+
Akaua wanaume wao wenye nguvu zaidi;+Aliharibu wanaume vijana wa Israeli.
32 Ijapokuwa hayo walitenda zambi hata zaidi+Na hawakukuwa na imani katika kazi zake za ajabu.+
33 Kwa hiyo akakomesha siku zao kama vile ni pumuzi tu,+Na miaka yao kwa mambo ya kushitukia yenye kuogopesha sana.
34 Lakini kila mara wakati alikuwa anawaua, walikuwa wanamutafuta;+Walirudia na kumutafuta Mungu,
35 Walikumbuka kwamba Mungu alikuwa Mwamba wao+Na kwamba Mungu Mwenye Kuwa Juu Zaidi alikuwa Mukombozi* wao.+
36 Lakini walijaribu kumudanganya kwa kinywa chaoNa kumuambia uongo kwa ulimi wao.
37 Moyo wao haukukuwa imara kumuelekea;+Na hawakukuwa waaminifu kwa agano lake.+
38 Lakini alikuwa mwenye rehema;+Alikuwa anasamehe* kosa lao na hakuwaharibu.+
Mara nyingi alizuia hasira yake+Kuliko kuchochea kasirani yake kali yote.
39 Kwa maana alikumbuka kwamba walikuwa wenye mwili wa nyama,+Upepo wenye unapita na haurudie.*
40 Walimuasi mara nyingi sana katika jangwa+Na walimuhuzunisha katika jangwa!+
41 Walimujaribu Mungu tena na tena,+Na wakamuhuzunisha* Mutakatifu wa Israeli.
42 Hawakukumbuka nguvu zake,*Siku yenye aliwaokoa* kutoka kwa mupinzani,+
43 Namna alionyesha alama zake kule Misri+Na miujiza yake katika eneo la Soani,
44 Na namna alibadilisha mifereji ya Muto Nile kuwa damu+Na hivyo hawangeweza kunywa maji ya mito yake midogo.
45 Alituma vikundi vya mainzi ili viwameze+Na vyura ili kuwaharibu.+
46 Mazao yao aliyapatia nzige wenye kula sana,Matunda ya kazi yao ya nguvu akayapatia nzige wenye kupatikana kwa wingi.+
47 Aliharibu mizabibu yao kwa mvua ya majiwe+Na miti yao ya mikuyu kwa majiwe ya mvua.
48 Aliua wanyama wao wa kubeba mizigo kwa mvua ya majiwe+Na mifugo yao kwa umeme wa radi.*
49 Alimwanga juu yao kasirani yake yenye kuwaka,Kasirani kali na hasira na taabu,Vikundi vya malaika wenye kuleta musiba.
50 Alitayarisha njia kwa ajili ya kasirani yake.
Hakuwalinda wasikufe;*Na aliwaua kwa ugonjwa wa kuambukiza.
51 Mwishowe alipiga na kuua wazaliwa wote wa kwanza wa Misri,+Mwanzo wa nguvu zao za uzazi katika mahema ya Hamu.
52 Kisha akapeleka watu wake inje kama kundi+Na kuwaongoza katika jangwa kama kundi la wanyama.
53 Aliwaongoza kwa usalama,Na hawakuogopa;+Bahari ilifunika maadui wao.+
54 Na aliwaleta katika eneo lake takatifu,+Eneo hili lenye milima lenye mukono wake wa kuume ulijipatia.+
55 Alifukuza mataifa kutoka mbele yao;+Akawagawia uriti kwa kamba ya kupimia;+Alifanya makabila ya Israeli yakae katika makao yao.+
56 Lakini waliendelea kushindana na* Mungu Mwenye Kuwa Juu Zaidi, na kumuasi;+Hawakusikiliza vikumbusho vyake.+
57 Pia walipotoka na walikuwa wadanganyifu kama mababu zao.+
Hawakutegemeka kama vile upinde wenye kuregea.+
58 Waliendelea kumukasirisha kupitia mahali pao pa juu,+Na walichochea kasirani yake kali* kupitia sanamu zao za kuchongwa.+
59 Mungu alisikia na kukasirika sana,+Kwa hiyo akakataa kabisa Israeli.
60 Mwishowe akaacha tabenakulo ya Shilo,+Hema kwenye alikaa kati ya wanadamu.+
61 Aliacha alama ya nguvu zake ipelekwe katika utekwa;Utukufu wake utiwe katika mukono wa adui.+
62 Alitoa watu wake ili wauawe kwa upanga+Naye akakasirikia sana uriti wake.
63 Moto uliteketeza kabisa wanaume wake vijana,Na mabikira wake hawakuimbiwa nyimbo za arusi.*
64 Makuhani wake waliuawa kwa upanga,+Na wajane wao wenyewe hawakulia.+
65 Kisha Yehova akaamuka kama vile kutoka katika usingizi,+Kama mwanaume mwenye nguvu+ mwenye anaamuka kisha divai kumutoka.
66 Naye akakimbiza maadui wake;+Akawapatisha haya ya kudumu.
67 Alikataa hema ya Yosefu;Hakuchagua kabila la Efraimu.
68 Lakini alichagua kabila la Yuda,+Mulima Sayuni, wenye anapenda.+
69 Alifanya patakatifu pake kuwa mahali pa kudumu kama mbingu,*+Kama dunia yenye amefanya kuwa imara milele.+
70 Alimuchagua Daudi+ mutumishi wakeNa kumutosha katika mazizi* ya kondoo,+
71 Alimutosha katika kazi ya kuchunga kondoo-dike wenye kunyonyesha;Akamufanya kuwa muchungaji juu ya Yakobo, watu wake,+Na juu ya Israeli, uriti wake.+
72 Aliwachunga kwa uaminifu-mushikamanifu wa moyo,+Na aliwaongoza kwa mikono yenye ufundi.+
Maelezo ya Chini
^ Angalia Maana ya Maneno.
^ Ao “agizo langu.”
^ Tnn., “wenye ulikuwa haujatayarishwa.”
^ Ao “ukuta.”
^ Tnn., “Walimujaribu.”
^ Ao “chakula kwa ajili ya nafsi yao.”
^ Ao “wa malaika.”
^ Ao “Mulipiza-Kisasi.”
^ Tnn., “anafunika.”
^ Ao pengine, “Kwamba roho inaenda na hairudie.”
^ Ao “wakamutia uchungu.”
^ Tnn., “mukono wake.”
^ Tnn., “aliwakomboa.”
^ Ao pengine, “homa kali.”
^ Ao “Hakulinda nafsi yao isikufe.”
^ Tnn., “kumujaribu.”
^ Ao “wivu wake.”
^ Tnn., “Na mabikira wake hawakusifiwa.”
^ Tnn., “Alijenga patakatifu pake kama nafasi za juu.”
^ Zizi ni lupango ya kuchungia wanyama.