Zaburi 113:1-9
113 Mumusifu Yah!*
Mumusifu, ninyi watumishi wa Yehova,Musifu jina la Yehova.
2 Jina la Yehova lisifiweKuanzia sasa na milele.+
3 Kuanzia mahali jua linatokea mupaka mahali jua linashukia,Jina la Yehova lisifiwe.+
4 Yehova iko* juu sana ya mataifa yote;+Utukufu wake uko juu ya mbingu.+
5 Ni nani mwenye kuwa kama Yehova Mungu wetu,+Mwenye anakaa* kule juu?
6 Anainama ili aangalie mbingu na dunia,+
7 Anainua mutu wa hali ya chini kutoka katika mavumbi.
Anainua maskini kutoka kwenye rundo la majivu*+
8 Ili kumufanya akae pamoja na watu wenye vyeo,Pamoja na watu wenye vyeo kati ya watu wake.
9 Anapatia makao mwanamuke tasaKama mama mwenye furaha mwenye kuwa na watoto.*+
Mumusifu Yah!*

