Zaburi 101:1-8
Ya Daudi. Muziki.
101 Nitaimba kuhusu upendo mushikamanifu na haki.
Nitakuimbia sifa,* Ee Yehova.
2 Nitatenda kwa busara na bila lawama.*
Utakuja kwangu wakati gani?
Nitatembea kwa uaminifu-mushikamanifu wa moyo+ ndani ya nyumba yangu.
3 Sitatia mbele ya macho yangu kitu chenye hakina mafaa yoyote.
Ninachukia matendo ya wale wenye kukengeuka na kuacha mambo yenye kuwa sawa;+Sitashirikiana nao hata kidogo.*
4 Moyo wenye kupotoka uko mbali na mimi;Sitakubali* mambo ya mubaya.
5 Mutu yeyote mwenye kumuchongea jirani yake kwa uficho,+Nitamunyamazisha.*
Mutu yeyote mwenye kuwa na macho yenye kiburi na moyo wenye majivuno,Sitamuvumilia.
6 Nitaangalia waaminifu wa dunia,Ili wakae pamoja na mimi.
Ule mwenye kutembea bila lawama* atanitumikia.
7 Hakuna mutu yeyote mudanganyifu mwenye atakaa katika nyumba yangu,Na hakuna muongo yeyote mwenye atasimama mbele yangu.*
8 Kila asubui nitanyamazisha* waovu wote wa dunia,Ili kuondoa wakosaji wote katika muji wa Yehova.+

