Zaburi 101:1-8

  • Mutawala mwenye kutenda kwa uaminifu-mushikamanifu

    • ‘Sitavumilia kiburi’ (5)

    • “Nitaangalia waaminifu” (6)

Ya Daudi. Muziki. 101  Nitaimba kuhusu upendo mushikamanifu na haki. Nitakuimbia sifa,* Ee Yehova.  2  Nitatenda kwa busara na bila lawama.* Utakuja kwangu wakati gani? Nitatembea kwa uaminifu-mushikamanifu wa moyo+ ndani ya nyumba yangu.  3  Sitatia mbele ya macho yangu kitu chenye hakina mafaa yoyote. Ninachukia matendo ya wale wenye kukengeuka na kuacha mambo yenye kuwa sawa;+Sitashirikiana nao hata kidogo.*  4  Moyo wenye kupotoka uko mbali na mimi;Sitakubali* mambo ya mubaya.  5  Mutu yeyote mwenye kumuchongea jirani yake kwa uficho,+Nitamunyamazisha.* Mutu yeyote mwenye kuwa na macho yenye kiburi na moyo wenye majivuno,Sitamuvumilia.  6  Nitaangalia waaminifu wa dunia,Ili wakae pamoja na mimi. Ule mwenye kutembea bila lawama* atanitumikia.  7  Hakuna mutu yeyote mudanganyifu mwenye atakaa katika nyumba yangu,Na hakuna muongo yeyote mwenye atasimama mbele yangu.*  8  Kila asubui nitanyamazisha* waovu wote wa dunia,Ili kuondoa wakosaji wote katika muji wa Yehova.+

Maelezo ya Chini

Ao “Nitakupigia muziki.”
Ao “kwa uaminifu-mushikamanifu.”
Ao “Matendo yao hayashikamane na mimi.”
Tnn., “Sitajua.”
Ao “Nitamuharibu.”
Ao “kwa uaminifu-mushikamanifu.”
Tnn., “mbele ya macho yangu.”
Ao “nitaharibu.”