Zaburi 23:1-6
Muziki wa Daudi.
23 Yehova ni Muchungaji wangu.+
Sitakosa kitu.+
2 Ananilalisha katika malisho yenye majani mengi;Ananiongoza kwenye nafasi za kupumuzikia zenye maji mengi.*+
3 Ananiburudisha.*+
Ananiongoza katika njia za* haki kwa ajili ya jina lake.+
4 Hata kama ninatembea katika bonde lenye kivuli kizito,+Siogope jambo lolote lenye kuumiza,+Kwa maana wewe uko pamoja na mimi;+Fimbo yako na gongo* yako vinanipatia uhakika.*
5 Unanitayarishia meza mbele ya maadui wangu.+
Unaburudisha* kichwa changu kwa mafuta;+Kikombe changu kimejazwa muzuri.+
6 Hakika wema na upendo mushikamanifu vitanifuata sikuzote za maisha yangu,+Na nitakaa katika nyumba ya Yehova siku zangu zote.+
Maelezo ya Chini
^ Ao pengine, “maji matulivu.”
^ Ao “Anaburudisha nafsi yangu.”
^ Tnn., “mapito yenye.”
^ Ao “vinanifariji.”
^ Gongo ni fimbo yenye kuvimba kwenye mwisho wake mumoja.
^ Ao “Unapakaa.”