Zaburi 23:1-6

  • “Yehova ni Muchungaji wangu”

    • “Sitakosa kitu” (1)

    • “Ananiburudisha” (3)

    • “Kikombe changu kimejazwa muzuri” (5)

Muziki wa Daudi. 23  Yehova ni Muchungaji wangu.+ Sitakosa kitu.+  2  Ananilalisha katika malisho yenye majani mengi;Ananiongoza kwenye nafasi za kupumuzikia zenye maji mengi.*+  3  Ananiburudisha.*+ Ananiongoza katika njia za* haki kwa ajili ya jina lake.+  4  Hata kama ninatembea katika bonde lenye kivuli kizito,+Siogope jambo lolote lenye kuumiza,+Kwa maana wewe uko pamoja na mimi;+Fimbo yako na gongo* yako vinanipatia uhakika.*  5  Unanitayarishia meza mbele ya maadui wangu.+ Unaburudisha* kichwa changu kwa mafuta;+Kikombe changu kimejazwa muzuri.+  6  Hakika wema na upendo mushikamanifu vitanifuata sikuzote za maisha yangu,+Na nitakaa katika nyumba ya Yehova siku zangu zote.+

Maelezo ya Chini

Ao pengine, “maji matulivu.”
Ao “Anaburudisha nafsi yangu.”
Tnn., “mapito yenye.”
Ao “vinanifariji.”
Gongo ni fimbo yenye kuvimba kwenye mwisho wake mumoja.
Ao “Unapakaa.”