Zaburi 56:1-13

  • Sala wakati mutu anateswa

    • “Katika Mungu ninaweka tegemeo langu” (4)

    • “Machozi yangu katika chupa yako ya ngozi” (8)

    • “Mwanadamu bure anaweza kunifanya nini?” (4,11)

Kwa kiongozi; imepatanishwa na “Njiwa Munyamavu Mwenye Kuwa Mbali.” Ya Daudi. Miktamu.* Wakati Wafilisti walimukamata kule Gati.+ 56  Unionyeshe wema, Ee Mungu, kwa sababu mwanadamu mwenye anaweza kufa ananishambulia.* Muchana wote wanaendelea kunipiga vita na kunikandamiza.  2  Maadui wangu wanatafuta kuniuma muchana wote;Wengi wanapigana na mimi kwa kiburi.  3  Wakati ninaogopa,+ ninakutegemea wewe.+  4  Katika Mungu⁠—​mwenye ninasifu neno lake⁠—Katika Mungu ninaweka tegemeo langu; siogope. Mwanadamu bure anaweza kunifanya* nini?+  5  Muchana wote wanaharibu mambo yangu;Jambo pekee lenye wanafikiria ni kunifanya mubaya.+  6  Wanajificha ili kushambulia,Wanachunguza kila hatua yangu,+Wakitumaini kuondoa uzima wangu.*+  7  Uwakatae kwa sababu ya uovu wao. Angusha mataifa kwa kasirani yako, Ee Mungu.+  8  Unafuatilia kutanga-tanga kwangu.+ Kusanya machozi yangu katika chupa yako ya ngozi.+ Je, hayaandikwe katika kitabu chako?+  9  Maadui wangu watakimbia siku yenye nitaomba musaada.+ Niko hakika na jambo hili: Mungu iko* upande wangu.+ 10  Katika Mungu⁠—​mwenye ninasifu neno lake⁠—Katika Yehova⁠—​mwenye ninasifu neno lake⁠— 11  Katika Mungu ninaweka tegemeo langu; siogope.+ Mwanadamu bure anaweza kunifanya nini?+ 12  Nimefungwa na naziri zenye niliweka kwako, Ee Mungu;+Nitakutolea maneno ya shukrani.+ 13  Kwa maana umeniokoa* katika kifo+Na umezuia miguu yangu isijikwae,+Ili nitembee mbele ya Mungu katika mwangaza wa wazima.+

Maelezo ya Chini

Ao “anataka kuniuma.”
Tnn., “Nyama inaweza kunifanya.”
Ao “nafsi yangu.”
Ao “eko.”
Ao “umeokoa nafsi yangu.”