Zaburi 56:1-13
Kwa kiongozi; imepatanishwa na “Njiwa Munyamavu Mwenye Kuwa Mbali.” Ya Daudi. Miktamu.* Wakati Wafilisti walimukamata kule Gati.+
56 Unionyeshe wema, Ee Mungu, kwa sababu mwanadamu mwenye anaweza kufa ananishambulia.*
Muchana wote wanaendelea kunipiga vita na kunikandamiza.
2 Maadui wangu wanatafuta kuniuma muchana wote;
Wengi wanapigana na mimi kwa kiburi.
3 Wakati ninaogopa,+ ninakutegemea wewe.+
4 Katika Mungu—mwenye ninasifu neno lake—
Katika Mungu ninaweka tegemeo langu; siogope.
Mwanadamu bure anaweza kunifanya* nini?+
5 Muchana wote wanaharibu mambo yangu;
Jambo pekee lenye wanafikiria ni kunifanya mubaya.+
6 Wanajificha ili kushambulia,
Wanachunguza kila hatua yangu,+
Wakitumaini kuondoa uzima wangu.*+
7 Uwakatae kwa sababu ya uovu wao.
Angusha mataifa kwa kasirani yako, Ee Mungu.+
8 Unafuatilia kutanga-tanga kwangu.+
Kusanya machozi yangu katika chupa yako ya ngozi.+
Je, hayaandikwe katika kitabu chako?+
9 Maadui wangu watakimbia siku yenye nitaomba musaada.+
Niko hakika na jambo hili: Mungu iko* upande wangu.+
10 Katika Mungu—mwenye ninasifu neno lake—
Katika Yehova—mwenye ninasifu neno lake—
11 Katika Mungu ninaweka tegemeo langu; siogope.+
Mwanadamu bure anaweza kunifanya nini?+
12 Nimefungwa na naziri zenye niliweka kwako, Ee Mungu;+
Nitakutolea maneno ya shukrani.+
13 Kwa maana umeniokoa* katika kifo+
Na umezuia miguu yangu isijikwae,+
Ili nitembee mbele ya Mungu katika mwangaza wa wazima.+
Maelezo ya Chini
^ Angalia Maana ya Maneno.
^ Ao “anataka kuniuma.”
^ Tnn., “Nyama inaweza kunifanya.”
^ Ao “nafsi yangu.”
^ Ao “eko.”
^ Ao “umeokoa nafsi yangu.”