Zaburi 56:1-13

  • Sala wakati mutu anateswa

    • “Katika Mungu ninaweka tegemeo langu” (4)

    • “Machozi yangu katika chupa yako ya ngozi” (8)

    • “Mwanadamu bure anaweza kunifanya nini?” (4, 11)

Kwa kiongozi; imepatanishwa na “Njiwa Munyamavu Mwenye Kuwa Mbali.” Ya Daudi. Miktamu.* Wakati Wafilisti walimukamata kule Gati.+ 56  Unionyeshe wema, Ee Mungu, kwa sababu mwanadamu mwenye anaweza kufa ananishambulia.* Muchana wote wanaendelea kunipiga vita na kunikandamiza.   Maadui wangu wanatafuta kuniuma muchana wote; Wengi wanapigana na mimi kwa kiburi.   Wakati ninaogopa,+ ninakutegemea wewe.+   Katika Mungu—mwenye ninasifu neno lake— Katika Mungu ninaweka tegemeo langu; siogope. Mwanadamu bure anaweza kunifanya* nini?+   Muchana wote wanaharibu mambo yangu; Jambo pekee lenye wanafikiria ni kunifanya mubaya.+   Wanajificha ili kushambulia, Wanachunguza kila hatua yangu,+ Wakitumaini kuondoa uzima wangu.*+   Uwakatae kwa sababu ya uovu wao. Angusha mataifa kwa kasirani yako, Ee Mungu.+   Unafuatilia kutanga-tanga kwangu.+ Kusanya machozi yangu katika chupa yako ya ngozi.+ Je, hayaandikwe katika kitabu chako?+   Maadui wangu watakimbia siku yenye nitaomba musaada.+ Niko hakika na jambo hili: Mungu iko* upande wangu.+ 10  Katika Mungu⁠—​mwenye ninasifu neno lake⁠— Katika Yehova⁠—​mwenye ninasifu neno lake⁠— 11  Katika Mungu ninaweka tegemeo langu; siogope.+ Mwanadamu bure anaweza kunifanya nini?+ 12  Nimefungwa na naziri zenye niliweka kwako, Ee Mungu;+ Nitakutolea maneno ya shukrani.+ 13  Kwa maana umeniokoa* katika kifo+ Na umezuia miguu yangu isijikwae,+ Ili nitembee mbele ya Mungu katika mwangaza wa wazima.+

Maelezo ya Chini

Ao “anataka kuniuma.”
Tnn., “Nyama inaweza kunifanya.”
Ao “nafsi yangu.”
Ao “eko.”
Ao “umeokoa nafsi yangu.”