Zaburi 40:1-17
Kwa kiongozi. Ya Daudi. Muziki.
40 Nilimutumainia Yehova kwa bidii,*Naye akanitegea sikio lake* na kusikia kilio changu cha kuomba musaada.+
2 Akanipandisha kutoka katika shimo lenye kunguruma,Kutoka katika matope yenye uterezi.
Akatia miguu yangu juu ya mwamba;Akanifanya nisimame mahali kwenye kuko salama.
3 Kisha akatia wimbo mupya katika kinywa changu,+Mungu wetu asifiwe.
Wengi wataangalia na kuogopa sanaNa kuweka tegemeo lao katika Yehova.
4 Mwenye furaha ni mutu mwenye anamutegemea YehovaNa mwenye hatumainie watu wenye wako kichwa-nguvu ao watu wadanganyifu.*
5 Mambo yenye umefanya ni mengi sana,Ee Yehova Mungu wangu,Kazi zako za ajabu na mawazo yako kutuelekea.+
Hakuna mwenye anaweza kulinganishwa na wewe;+Kama ningejaribu kueleza na kuongea kuzihusu,Zingekuwa nyingi sana kwangu kusimulia!+
6 Haukutamani* zabihu na toleo,+Lakini ulifungua masikio yangu ili yasikie.+
Haukuomba matoleo ya kuteketezwa na matoleo ya zambi.+
7 Kisha nikasema: “Angalia, nimekuja.
Katika kitabu cha kukunjwa* imeandikwa juu yangu.+
8 Ee Mungu wangu, ninafurahia* kufanya mapenzi yako,+Na sheria yako iko ndani yangu kabisa.+
9 Ninatangaza habari njema ya haki katika kutaniko kubwa.+
Angalia! Sizuie midomo yangu,+Ee Yehova, kama vile unajua muzuri.
10 Sifunike haki yako katika moyo wangu.
Ninatangaza uaminifu wako na wokovu wako.
Sifiche upendo wako mushikamanifu na kweli yako katika kutaniko kubwa.”+
11 Ee Yehova, usiniime rehema yako.
Upendo wako mushikamanifu na kweli yako vinilinde kila wakati.+
12 Misiba yenye kunizunguka ni mingi sana haiwezi kuhesabika.+
Makosa yangu mengi yananilemea kiasi ya kwamba siwezi kuona njia yangu;+Ni mengi sana kuliko nywele za kichwa changu,Na nimevunjika moyo.
13 Tafazali, Ee Yehova, ukuwe tayari kuniokoa.+
Ee Yehova, fanya haraka ili unisaidie.+
14 Acha wale wote wenye kutafuta kuondoa uzima wangu*Wapatishwe haya na kufezeheshwa.
Acha wale wenye kufurahia musiba wanguWakimbie kwa sababu ya aibu.
15 Acha wale wenye kuniambia: “Aha! Aha!”
Washituke kwa sababu ya haya yao wenyewe.
16 Lakini acha wale wenye kukutafuta+Wafurahi na kushangilia katika wewe.+
Acha wale wenye kupenda matendo yako ya wokovu waseme sikuzote:
“Yehova atukuzwe.”+
17 Lakini mimi sina uwezo, na niko maskini;Yehova anikazie uangalifu.
Wewe ni musaidizi wangu na mwokozi wangu;+Mungu wangu, usikawie.+

