Zaburi 40:1-17

  • Kumushukuru Mungu mwenye hawezi kulinganishwa na mutu yeyote

    • Kazi za Mungu ni nyingi sana haziwezi kusimuliwa (5)

    • Haiko zabihu ndizo Mungu anahangaikia kwanza (6)

    • “Ninafurahia kufanya mapenzi yako” (8)

Kwa kiongozi. Ya Daudi. Muziki. 40  Nilimutumainia Yehova kwa bidii,* Naye akanitegea sikio lake* na kusikia kilio changu cha kuomba musaada.+   Akanipandisha kutoka katika shimo lenye kunguruma, Kutoka katika matope yenye uterezi. Akatia miguu yangu juu ya mwamba; Akanifanya nisimame mahali kwenye kuko salama.   Kisha akatia wimbo mupya katika kinywa changu,+ Mungu wetu asifiwe. Wengi wataangalia na kuogopa sana Na kuweka tegemeo lao katika Yehova.   Mwenye furaha ni mutu mwenye anamutegemea Yehova Na mwenye hatumainie watu wenye wako kichwa-nguvu ao watu wadanganyifu.*   Mambo yenye umefanya ni mengi sana, Ee Yehova Mungu wangu, Kazi zako za ajabu na mawazo yako kutuelekea.+ Hakuna mwenye anaweza kulinganishwa na wewe;+ Kama ningejaribu kueleza na kuongea kuzihusu, Zingekuwa nyingi sana kwangu kusimulia!+   Haukutamani* zabihu na toleo,+ Lakini ulifungua masikio yangu ili yasikie.+ Haukuomba matoleo ya kuteketezwa na matoleo ya zambi.+   Kisha nikasema: “Angalia, nimekuja. Katika kitabu cha kukunjwa* imeandikwa juu yangu.+   Ee Mungu wangu, ninafurahia* kufanya mapenzi yako,+ Na sheria yako iko ndani yangu kabisa.+   Ninatangaza habari njema ya haki katika kutaniko kubwa.+ Angalia! Sizuie midomo yangu,+ Ee Yehova, kama vile unajua muzuri. 10  Sifunike haki yako katika moyo wangu. Ninatangaza uaminifu wako na wokovu wako. Sifiche upendo wako mushikamanifu na kweli yako katika kutaniko kubwa.”+ 11  Ee Yehova, usiniime rehema yako. Upendo wako mushikamanifu na kweli yako vinilinde kila wakati.+ 12  Misiba yenye kunizunguka ni mingi sana haiwezi kuhesabika.+ Makosa yangu mengi yananilemea kiasi ya kwamba siwezi kuona njia yangu;+ Ni mengi sana kuliko nywele za kichwa changu, Na nimevunjika moyo. 13  Tafazali, Ee Yehova, ukuwe tayari kuniokoa.+ Ee Yehova, fanya haraka ili unisaidie.+ 14  Acha wale wote wenye kutafuta kuondoa uzima wangu* Wapatishwe haya na kufezeheshwa. Acha wale wenye kufurahia musiba wangu Wakimbie kwa sababu ya aibu. 15  Acha wale wenye kuniambia: “Aha! Aha!” Washituke kwa sababu ya haya yao wenyewe. 16  Lakini acha wale wenye kukutafuta+ Wafurahi na kushangilia katika wewe.+ Acha wale wenye kupenda matendo yako ya wokovu waseme sikuzote: “Yehova atukuzwe.”+ 17  Lakini mimi sina uwezo, na niko maskini; Yehova anikazie uangalifu. Wewe ni musaidizi wangu na mwokozi wangu;+ Mungu wangu, usikawie.+

Maelezo ya Chini

Ao “Nilimungojea Yehova kwa uvumilivu.”
Ao “akainama chini ili kunisikiliza.”
Ao “waongo.”
Ao “Haukupendezwa na.”
Tnn., “mukunjo wa kitabu.”
Ao “ninatamani.”
Ao “nafsi yangu.”