Zaburi 116:1-19

  • Wimbo wa shukrani

    • “Nitamulipa Yehova nini?” (12)

    • “Nitainua kikombe cha wokovu” (13)

    • “Nitamutimizia Yehova naziri zangu” (14, 18)

    • Kifo cha washikamanifu ni chenye bei kali (15)

116  Ninamupenda Yehova Kwa sababu anasikia* sauti yangu, vilio vyangu vya kuomba musaada.+   Kwa maana ananitegea sikio lake,*+ Na nitamuitia wakati wote wenye nitakuwa muzima.*   Kamba za kifo zilinizunguka; Kaburi lilinishika kwa nguvu.*+ Nililemewa na taabu na huzuni.+   Lakini niliitia jina la Yehova:+ “Ee, Yehova, niokoe!”*   Yehova ni mwenye huruma* na mwenye haki;+ Mungu wetu ni mwenye rehema.+   Yehova analinda wenye hawana uzoefu.+ Nilishushwa chini, na aliniokoa.   Acha nafsi* yangu ipumuzike tena, Kwa maana Yehova amenitendea kwa fazili.   Umeniokoa* kutoka katika kifo, Jicho langu kutokana na machozi, muguu wangu kutokana na kujikwaa.+   Nitatembea mbele ya Yehova katika inchi ya wazima. 10  Nilikuwa na imani, ndio maana nilisema;+ Niliteseka sana. 11  Sasa mimi, niliogopa na kusema: “Kila mwanadamu ni muongo.”+ 12  Nitamulipa Yehova nini Kwa mema yote yenye amenitendea? 13  Nitainua kikombe cha wokovu,* Na nitaitia jina la Yehova. 14  Nitamutimizia Yehova naziri zangu Mbele ya watu wake wote.+ 15  Ni chenye bei kali* mbele ya macho ya Yehova Kifo cha washikamanifu wake.+ 16  Ninakulilia, Ee Yehova, Kwa maana mimi ni mutumishi wako. Mimi ni mutumishi wako, mwana wa mutumwa wako mwanamuke. Umenifungua katika vifungo vyangu.+ 17  Nitakutolea zabihu ya shukrani;+ Nitaitia jina la Yehova. 18  Nitamutimizia Yehova naziri zangu+ Mbele ya watu wake wote,+ 19  Katika viwanja vya nyumba ya Yehova,+ Katikati yako, Ee Yerusalemu. Mumusifu Yah!*+

Maelezo ya Chini

Ao pengine, “Ninapenda kwa sababu Yehova anasikia.”
Ao “anainama chini ili kunisikiliza.”
Tnn., “katika siku zangu.”
Tnn., “Taabu za Sheoli zilinipata.”
Ao “okoa nafsi yangu.”
Ao “neema.”
Ao “Umeokoa nafsi yangu.”
Ao “wokovu mukubwa.”
Tnn., “chenye samani.”
Ao “Haleluya!” “Yah” ni kifupi cha jina Yehova.