Zaburi 116:1-19
116 Ninamupenda YehovaKwa sababu anasikia* sauti yangu, vilio vyangu vya kuomba musaada.+
2 Kwa maana ananitegea sikio lake,*+Na nitamuitia wakati wote wenye nitakuwa muzima.*
3 Kamba za kifo zilinizunguka;Kaburi lilinishika kwa nguvu.*+
Nililemewa na taabu na huzuni.+
4 Lakini niliitia jina la Yehova:+
“Ee, Yehova, niokoe!”*
5 Yehova ni mwenye huruma* na mwenye haki;+Mungu wetu ni mwenye rehema.+
6 Yehova analinda wenye hawana uzoefu.+
Nilishushwa chini, na aliniokoa.
7 Acha nafsi* yangu ipumuzike tena,Kwa maana Yehova amenitendea kwa fazili.
8 Umeniokoa* kutoka katika kifo,Jicho langu kutokana na machozi, muguu wangu kutokana na kujikwaa.+
9 Nitatembea mbele ya Yehova katika inchi ya wazima.
10 Nilikuwa na imani, ndio maana nilisema;+Niliteseka sana.
11 Sasa mimi, niliogopa na kusema:
“Kila mwanadamu ni muongo.”+
12 Nitamulipa Yehova niniKwa mema yote yenye amenitendea?
13 Nitainua kikombe cha wokovu,*Na nitaitia jina la Yehova.
14 Nitamutimizia Yehova naziri zanguMbele ya watu wake wote.+
15 Ni chenye bei kali* mbele ya macho ya YehovaKifo cha washikamanifu wake.+
16 Ninakulilia, Ee Yehova,Kwa maana mimi ni mutumishi wako.
Mimi ni mutumishi wako, mwana wa mutumwa wako mwanamuke.
Umenifungua katika vifungo vyangu.+
17 Nitakutolea zabihu ya shukrani;+Nitaitia jina la Yehova.
18 Nitamutimizia Yehova naziri zangu+Mbele ya watu wake wote,+
19 Katika viwanja vya nyumba ya Yehova,+Katikati yako, Ee Yerusalemu.
Mumusifu Yah!*+
Maelezo ya Chini
^ Ao pengine, “Ninapenda kwa sababu Yehova anasikia.”
^ Ao “anainama chini ili kunisikiliza.”
^ Tnn., “katika siku zangu.”
^ Tnn., “Taabu za Sheoli zilinipata.”
^ Ao “okoa nafsi yangu.”
^ Ao “neema.”
^ Angalia Maana ya Maneno.
^ Ao “Umeokoa nafsi yangu.”
^ Ao “wokovu mukubwa.”
^ Tnn., “chenye samani.”
^ Ao “Haleluya!” “Yah” ni kifupi cha jina Yehova.

