Zaburi 120:1-7

  • Mugeni anatamani amani

    • ‘Uniokoe kutokana na ulimi mudanganyifu’ (2)

    • “Mimi ni mutu wa amani” (7)

Wimbo wa Safari za Kupanda.* 120  Nilimuita Yehova katika taabu yangu,+Na akanijibu.+  2  Ee Yehova, niokoe* kutokana na midomo yenye kusema uongoNa kutokana na ulimi mudanganyifu.  3  Atakufanya nini, Naye atakupatia azabu namna gani,*Wewe ulimi mudanganyifu?+  4  Kwa mishale mikali+ ya mupiganaji-vitaNa makaa yenye kuwaka+ ya miti ya miretemu.  5  Ole wangu, kwa maana nimeishi kama mugeni katika Mesheki!+ Nimekuwa nikiishi kati ya mahema ya Kedari.+  6  Nimekuwa nikiishi* kwa wakati murefu sanaPamoja na wale wenye kuchukia amani.+  7  Mimi ni mutu wa amani, lakini wakati ninasema,Wao wanataka vita.

Maelezo ya Chini

Ao “okoa nafsi yangu.”
Tnn., “Naye atakuongezea nini?”
Ao “Nafsi yangu imekuwa ikiishi.”