Zaburi 120:1-7
Wimbo wa Safari za Kupanda.*
120 Nilimuita Yehova katika taabu yangu,+Na akanijibu.+
2 Ee Yehova, niokoe* kutokana na midomo yenye kusema uongoNa kutokana na ulimi mudanganyifu.
3 Atakufanya nini, Naye atakupatia azabu namna gani,*Wewe ulimi mudanganyifu?+
4 Kwa mishale mikali+ ya mupiganaji-vitaNa makaa yenye kuwaka+ ya miti ya miretemu.
5 Ole wangu, kwa maana nimeishi kama mugeni katika Mesheki!+
Nimekuwa nikiishi kati ya mahema ya Kedari.+
6 Nimekuwa nikiishi* kwa wakati murefu sanaPamoja na wale wenye kuchukia amani.+
7 Mimi ni mutu wa amani, lakini wakati ninasema,Wao wanataka vita.
Maelezo ya Chini
^ Angalia Maana ya Maneno.
^ Ao “okoa nafsi yangu.”
^ Tnn., “Naye atakuongezea nini?”
^ Ao “Nafsi yangu imekuwa ikiishi.”

