Zaburi 149:1-9
149 Mumusifu Yah!*
Mumuimbie Yehova wimbo mupya;+Mumusifu katika kutaniko la washikamanifu.+
2 Israeli ashangilie katika Mutengenezaji wake Mukubwa;+Wana wa Sayuni wafurahi katika Mufalme wao.
3 Wasifu jina lake kwa kucheza dansi+Na wamuimbie sifa* kwa ngoma ya kidogo* na kinubi.+
4 Kwa maana Yehova anafurahia watu wake.+
Anapamba wapole kwa wokovu.+
5 Washikamanifu washangilie kwa utukufu;Wapige vigelegele vya shangwe kwenye vitanda vyao.+
6 Nyimbo za kumusifu Mungu zikuwe katika koo yao,Na upanga wenye makali pande mbili ukuwe katika mukono wao,
7 Ili kulipiza kisasi juu ya mataifaNa kupatia vikundi vya watu azabu,
8 Ili kufunga wafalme wao kwa minyororoNa watu wao wenye vyeo kwa pingu za chuma,
9 Ili kuleta hukumu yenye iliandikwa kwa ajili yao.+
Heshima hii ni ya washikamanifu wake wote.
Mumusifu Yah!*

