Zaburi 149:1-9

  • Wimbo wa kusifu ushindi wa Mungu

    • Mungu anafurahia watu wake (4)

    • Heshima ni ya washikamanifu wa Mungu (9)

149  Mumusifu Yah!* Mumuimbie Yehova wimbo mupya;+Mumusifu katika kutaniko la washikamanifu.+  2  Israeli ashangilie katika Mutengenezaji wake Mukubwa;+Wana wa Sayuni wafurahi katika Mufalme wao.  3  Wasifu jina lake kwa kucheza dansi+Na wamuimbie sifa* kwa ngoma ya kidogo* na kinubi.+  4  Kwa maana Yehova anafurahia watu wake.+ Anapamba wapole kwa wokovu.+  5  Washikamanifu washangilie kwa utukufu;Wapige vigelegele vya shangwe kwenye vitanda vyao.+  6  Nyimbo za kumusifu Mungu zikuwe katika koo yao,Na upanga wenye makali pande mbili ukuwe katika mukono wao,  7  Ili kulipiza kisasi juu ya mataifaNa kupatia vikundi vya watu azabu,  8  Ili kufunga wafalme wao kwa minyororoNa watu wao wenye vyeo kwa pingu za chuma,  9  Ili kuleta hukumu yenye iliandikwa kwa ajili yao.+ Heshima hii ni ya washikamanifu wake wote. Mumusifu Yah!*

Maelezo ya Chini

Ao “Haleluya!” “Yah” ni kifupi cha jina Yehova.
Ao “wamupigie muziki.”
Ao “tari.”
Ao “Haleluya!” “Yah” ni kifupi cha jina Yehova.