Zaburi 52:1-9

  • Kutegemea upendo mushikamanifu wa Mungu

    • Wenye kujisifu kwa sababu ya ubaya wanaonywa (1-5)

    • Wenye hawamuogope Mungu wanategemea utajiri (7)

Kwa kiongozi. Maskili.* Ya Daudi, wakati Doegi Mwedomu alikuja na kumuambia Sauli kwamba Daudi alikuwa ameenda kwenye nyumba ya Ahimeleki.+ 52  Sababu gani unajisifu kuhusu matendo yako maovu, wewe mwenye nguvu?+ Upendo mushikamanifu wa Mungu unadumu muchana wote.+  2  Ulimi wako, wenye makali kama wembe,+Unapanga mambo yenye kuumiza na kutenda kwa udanganyifu.+  3  Unapenda uovu kuliko mema,Kusema uongo kuliko kusema mambo yenye kuwa sawa. (Sela)  4  Unapenda kila neno lenye kuumiza,Ee ulimi mudanganyifu!  5  Ndiyo sababu Mungu atakubomoa milele na milele;+Atakukamata haraka na kukupasua kutoka katika hema yako;+Atakungoa kutoka katika inchi ya wazima.+ (Sela)  6  Wenye haki wataona jambo hilo na kujaa woga mukubwa,+Na watamucheka.+  7  “Huyu ndiye mwanaume mwenye hakumufanya Mungu kuwa kimbilio lake,*+Lakini alitumainia utajiri wake mwingi+Na alitegemea* mipango yake mwenyewe ya uovu.”*  8  Lakini mimi nitakuwa kama muzeituni wenye majani mengi katika nyumba ya Mungu;Ninategemea upendo mushikamanifu wa Mungu,+ milele na milele.  9  Nitakusifu milele kwa sababu umekamata hatua;+Mbele ya washikamanifu wako,Nitatumainia jina lako,+ kwa maana ni muzuri.

Maelezo ya Chini

Ao “ngome yake.”
Ao “kujificha katika.”
Tnn., “taabu zenye analeta.”