Zaburi 94:1-23
94 Ee Mungu wa kisasi, Yehova,+
Ee Mungu wa kisasi, angaza!
2 Simama, Ee Muamuzi wa dunia.+
Lipa wenye majivuno kile wanastahili.+
3 Waovu wataendelea mupaka wakati gani, Ee Yehova,
Waovu wataendelea kushangilia mupaka wakati gani?+
4 Wanasema maneno mengi yenye hayana maana na kuongea kwa kiburi;
Wakosaji wote wanajisifu.
5 Wanaponda watu wako, Ee Yehova,+
Na kukandamiza uriti wako.
6 Wanaua mujane na mukaaji mugeni,
Na kuua watoto wenye hawana baba.
7 Wanasema: “Yah haone;+
Mungu wa Yakobo hatambue jambo hilo.”+
8 Muelewe jambo hili, ninyi wenye hamuna akili;
Ninyi wapumbavu, ni wakati gani mutaonyesha ufahamu?+
9 Ule mwenye alifanya* sikio, je, hawezi kusikia?
Ule mwenye aliumba jicho, je, hawezi kuona?+
10 Ule mwenye kurekebisha mataifa, je, hawezi kukaripia?+
Yeye Ndiye anafundisha watu ujuzi!+
11 Yehova anajua mawazo ya wanadamu,
Kwamba ni pumuzi tu.+
12 Mwenye furaha ni mutu mwenye unarekebisha, Ee Yah,+
Mwenye unafundisha mambo yenye kuwa katika sheria yako,+
13 Ili kumupatia utulivu katika siku za musiba,
Mupaka wakati shimo litachimbwa kwa ajili ya waovu.+
14 Kwa maana Yehova hataacha watu wake,+
Wala kutupa uriti wake.+
15 Kwa maana hukumu itakuwa tena yenye haki,
Na wote wenye kuwa wanyoofu katika moyo wataifuata.
16 Ni nani atasimama ili kushambulia waovu kwa ajili yangu?
Ni nani atanitetea juu ya wakosaji?
17 Kama Yehova hangekuwa musaidizi wangu,
Kisha wakati kidogo tu ningekuwa nimekufa.*+
18 Wakati nilisema: “Muguu wangu unatereza,”
Upendo wako mushikamanifu, Ee Yehova, uliendelea kunitegemeza.+
19 Wakati mahangaiko* yalinilemea,*
Ulinifariji na kunituliza.*+
20 Je, kiti cha ufalme chenye upotovu kinaweza* kuungana na wewe
Wakati kinatunga matatizo kwa kutumia sheria?*+
21 Wanashambulia kwa ukali mwenye haki*+
Na kumuhukumia kifo mutu mwenye hana kosa.*+
22 Lakini Yehova atakuwa kimbilio langu salama,*
Mungu wangu ni mwamba wangu wenye ninakimbilia.+
23 Atafanya matendo yao maovu yawarudilie.+
Atawaharibu* kupitia uovu wao wenyewe.
Yehova Mungu wetu atawaharibu.*+
Maelezo ya Chini
^ Tnn., “alipanda.”
^ Tnn., “nafsi yangu ingekuwa imekaa katika ukimya.”
^ Ao “mawazo yenye kusumbua.”
^ Ao “yalikuwa mengi ndani yangu.”
^ Ao “Faraja zako zilituliza nafsi yangu.”
^ Ao “watawala wenye upotovu wanaweza; waamuzi wenye upotovu wanaweza.”
^ Ao “kwa njia ya amri.”
^ Tnn., “Na damu ya mwenye hana kosa wanaitangaza kuwa na hatia (yenye uovu).”
^ Ao “nafsi ya mwenye haki.”
^ Ao “mahali pangu salama pa juu.”
^ Tnn., “Atawanyamazisha.”
^ Tnn., “atawanyamazisha.”