UJIFUNZE BIBLIA NA MWALIMU
Furahia Maisha Milele!
Utajifunza Biblia kwa njia ya mazungumuzo, na bila kulipa. Na utapata majibu ya maulizo sawa vile:
Naweza kufanya nini juu nikuwe na furaha mu maisha?
Mambo ya mubaya na mateso itaishaka?
Nitaonaka tena watu wa familia na marafiki wangu wenye walishakufa?
Mungu ananihangaikia kabisa?
Napaswa kusali namna gani juu Mungu anisikie?
Haiko ya kulipia
Utajifunza Biblia bila kulipa, utapewa kitabu ya funzo Furahia Maisha Milele! bila kulipa na Biblia kama unapenda.
Utajifunza fasi, wakati, na mu namna yenye unapenda
Unaweza kuchagua kujifunza na mwalimu uso kwa uso, ao kupitia Enternete, fasi kwenye unapenda.
Uko huru
Unaweza kuamua kuacha kujifunza wakati unapenda; uko huru.
Tunajifunzaka Biblia namna gani?
Mwalimu atakusaidia kujua mambo yenye Biblia inafundisha. Mutajifunza habari fulani, kisha ingine. Wakati utaendelea kujifunza kitabu Furahia Maisha Milele!, pole kwa pole utavumbula mambo yenye Biblia inazungumuzia na namna inaweza kukusaidia. Juu ya kujua mambo mingi zaidi, angalia hii video ao soma majibu ya maulizo yenye watu wanauliza sana kuhusu programu yetu ya kujifunza Biblia.
Unapenda kupima?
Finyanga hapa chini juu ya kupanga mazungumuzo yako ya kwanza ya kujifunza Biblia.