Ona video zinazopatikana


UJIFUNZE BIBLIA NA MWALIMU

Furahia Maisha Milele!

Utajifunza Biblia kwa njia ya mazungumuzo, na bila kulipa. Na utapata majibu ya maulizo sawa vile:

  • Naweza kufanya nini juu nikuwe na furaha mu maisha?

  • Mambo ya mubaya na mateso itaishaka?

  • Nitaonaka tena watu wa familia na marafiki wangu wenye walishakufa?

  • Mungu ananihangaikia kabisa?

  • Napaswa kusali namna gani juu Mungu anisikie?

Haiko ya kulipia

Utajifunza Biblia bila kulipa, utapewa kitabu ya funzo Furahia Maisha Milele! bila kulipa na Biblia kama unapenda.

Utajifunza fasi, wakati, na mu namna yenye unapenda

Unaweza kuchagua kujifunza na mwalimu uso kwa uso, ao kupitia Enternete, fasi kwenye unapenda.

Uko huru

Unaweza kuamua kuacha kujifunza wakati unapenda; uko huru.

Namna gani utajifunza?

Mwalimu atakusaidia kujifunza mambo yenye Biblia inafundisha. Mutakuwa munajifunza habari moya kisha ingine. Mutakuwa munajifunza Biblia mu njia ya mazungumuzo kwa kutumia kitabu Furahia Maisha Milele! Kisha wakati fulani, utafikia kujua muzuri ujumbe wenye kuwa mu Biblia na namna unaweza kukusaidia. Juu upate habari zaidi, angalia hii video ao soma majibu ya maulizo yenye watu wanajiulizaka juu ya hii programu ya funzo.

Unapenda kupata wazo kidogo juu ya hii programu ya funzo?

Ona somo zenye kuwa ku mwanzo.

Uko tayari kupima?

Finya bouton juu upange sehemu ya kwanza ya funzo yako ya Biblia.