Zaburi 13:1-6

  • Kutamani wokovu wa Yehova

    • ‘Ee Yehova, mupaka wakati gani?’ (1, 2)

    • Yehova anatoa zawabu nyingi (6)

Kwa kiongozi. Muziki wa Daudi. 13  Ee Yehova, utanisahau mupaka wakati gani? Milele? Utanificha uso wako mupaka wakati gani?+  2  Nitahangaika* kwa wasiwasi mupaka wakati gani,Nikiwa na huzuni katika moyo wangu kila siku? Adui yangu atanishinda mupaka wakati gani?+  3  Uniangalie na unijibu, Ee Yehova Mungu wangu. Upatie macho yangu mwangaza, ili nisilale usingizi katika kifo,  4  Ili adui yangu asiseme: “Nimemushinda!” Usiruhusu wapinzani wangu washangilie kuanguka kwangu.+  5  Lakini mimi, ninategemea upendo wako mushikamanifu;+Moyo wangu utashangilia katika matendo yako ya wokovu.+  6  Nitamuimbia Yehova, kwa maana amenipatia zawabu nyingi.*+

Maelezo ya Chini

Ao “Nafsi yangu itahangaika.”
Ao “amenitendea kwa ukarimu.”