Zaburi 86:1-17
Sala ya Daudi.
86 Tega sikio lako,* Ee Yehova, na unijibu,Kwa maana ninateseka na niko maskini.+
2 Linda uzima wangu,* kwa maana niko mushikamanifu.+
Okoa mutumishi wako mwenye anakutegemea,Kwa maana wewe ni Mungu wangu.+
3 Unionyeshe wema, Ee Yehova,+Kwa maana ninakuita muchana wote.+
4 Fanya mutumishi wako ashangilie,*Kwa maana ninageuka kukuelekea wewe,* Ee Yehova.
5 Kwa maana wewe, Ee Yehova, uko mwema+ na uko tayari kusamehe;+Uko na upendo mwingi mushikamanifu kwa ajili ya wale wote wenye wanakuitia.+
6 Ee Yehova, sikiliza sala yangu;Na usikilize vilio vyangu vya kuomba musaada.+
7 Ninakuitia katika siku ya taabu yangu,+Kwa maana utanijibu.+
8 Hakuna mutu yeyote mwenye kuwa kama wewe kati ya miungu, Ee Yehova,+Hakuna kazi zenye kuwa kama kazi zako.+
9 Mataifa yote yenye ulifanyaYatakuja na kuinama mbele yako, Ee Yehova,+Na yatatukuza jina lako.+
10 Kwa maana uko mukubwa, na unafanya mambo ya ajabu;+Uko Mungu, wewe peke yako.+
11 Unifundishe, Ee Yehova, kuhusu njia yako.+
Nitatembea katika kweli yako.+
Unganisha moyo wangu* ili niogope jina lako.+
12 Ninakusifu, Ee Yehova Mungu wangu, kwa moyo wangu wote,+Na nitatukuza jina lako milele,
13 Kwa maana upendo wako mushikamanifu ni mwingi kunielekea,Na umeokoa uzima wangu* katika sehemu za chini kabisa za Kaburi.*+
14 Ee Mungu, watu wenye kimbelembele wanasimama ili kunishambulia;+Kikundi cha wanaume wenye hawana huruma kinatafuta kuondoa uzima wangu,*Na hawakuheshimie hata kidogo.*+
15 Lakini wewe, Ee Yehova, uko Mungu mwenye rehema na huruma,*Haukasirike haraka na uko mwenye upendo mwingi mushikamanifu na uaminifu.*+
16 Geuka kunielekea na unionyeshe wema.+
Patia mutumishi wako nguvu zako,+Na umuokoe mwana wa mutumwa wako mwanamuke.
17 Unionyeshe alama ya* wema wako,Ili wale wenye kunichukia waione na kupatishwa haya.
Kwa maana wewe, Ee Yehova, uko musaidizi wangu na mufariji wangu.
Maelezo ya Chini
^ Ao “Inama chini na unisikilize.”
^ Ao “nafsi yangu.”
^ Ao “nafsi ya mutumishi wako ishangilie.”
^ Ao “ninakuinulia nafsi yangu.”
^ Ao “Nipatie moyo wenye haugawanyike.”
^ Ao “Sheoli,” ni kusema, kaburi la wanadamu wote. Angalia Maana ya Maneno.
^ Ao “nafsi yangu.”
^ Ao “kinatafuta nafsi yangu.”
^ Ao “hawakukuweka mbele yao.”
^ Ao “neema.”
^ Ao “kweli.”
^ Ao “uhakikisho wa.”

