Zaburi 130:1-8
Wimbo wa Safari za Kupanda.
130 Ninakuita nikiwa katika sehemu za chini kabisa, Ee Yehova.+
2 Ee Yehova, sikia sauti yangu.
Masikio yako yasikilize vilio vyangu vya kuomba musaada.
3 Kama ungekuwa unaangalia* makosa, Ee Yah,*Basi ni nani, Ee Yehova, angeweza kusimama?+
4 Kwa maana wewe unatoa musamaha wa kweli,+Ili wakuogope sana.*+
5 Ninamutumainia Yehova, nafsi yangu yote inamutumainia;Ninangojea neno lake.
6 Ninamungojea* Yehova kwa hamu,+Kuliko namna walinzi wanangojea asubui,+Ndiyo, kuliko namna walinzi wanangojea asubui.
7 Israeli aendelee kumungojea Yehova,Kwa maana Yehova ni mushikamanifu katika upendo wake,+Na iko* na nguvu nyingi za kukomboa.
8 Atakomboa Israeli katika makosa yao yote.

