Zaburi 130:1-8

  • “Ninakuita nikiwa katika sehemu za chini kabisa”

    • ‘Kama ungekuwa unaangalia makosa’ (3)

    • Yehova anatoa musamaha wa kweli (4)

    • “Ninamungojea Yehova kwa hamu” (6)

Wimbo wa Safari za Kupanda. 130  Ninakuita nikiwa katika sehemu za chini kabisa, Ee Yehova.+  2  Ee Yehova, sikia sauti yangu. Masikio yako yasikilize vilio vyangu vya kuomba musaada.  3  Kama ungekuwa unaangalia* makosa, Ee Yah,*Basi ni nani, Ee Yehova, angeweza kusimama?+  4  Kwa maana wewe unatoa musamaha wa kweli,+Ili wakuogope sana.*+  5  Ninamutumainia Yehova, nafsi yangu yote inamutumainia;Ninangojea neno lake.  6  Ninamungojea* Yehova kwa hamu,+Kuliko namna walinzi wanangojea asubui,+Ndiyo, kuliko namna walinzi wanangojea asubui.  7  Israeli aendelee kumungojea Yehova,Kwa maana Yehova ni mushikamanifu katika upendo wake,+Na iko* na nguvu nyingi za kukomboa.  8  Atakomboa Israeli katika makosa yao yote.

Maelezo ya Chini

Ao “unafuatilia.”
“Yah” ni kifupi cha jina Yehova.
Tnn., “Ili wakuogope.”
Ao “Nafsi yangu inamungojea.”
Ao “eko.”