Zaburi 4:1-8

  • Sala ya kumutegemea Mungu

    • “Mukasirike, lakini musitende zambi” (4)

    • ‘Nitalala usingizi kwa amani’ (8)

Kwa kiongozi; iimbwe kwa vyombo vya kamba. Muziki wa Daudi. 4  Wakati ninakuita, unijibu, Ee Mungu wangu mwenye haki.+ Unitengenezee njia ya kuponyoka* taabu yangu. Unionyeshe wema na usikie sala yangu.  2  Ninyi wana wa binadamu, mutaendelea mupaka wakati gani kugeuza heshima yangu kuwa haya? Mutaendelea mupaka wakati gani kupenda mambo yenye hayana mafaa yoyote na kutafuta mambo ya uongo? (Sela)  3  Mujue kwamba Yehova atamutendea mushikamanifu wake kwa njia ya pekee;*Yehova atasikia wakati nitamuita.  4  Mukasirike, lakini musitende zambi.+ Museme katika moyo wenu, kwenye kitanda chenu, na munyamaze kimya. (Sela)  5  Mutoe zabihu za haki,Na mumutegemee Yehova.+  6  Kuko watu wengi wenye kusema: “Ni nani atatuonyesha jambo lolote la muzuri?” Mwangaza wa uso wako utuangazie, Ee Yehova.+  7  Umejaza moyo wangu shangwe nyingi sanaKuliko wale wenye kuwa na mavuno mengi sana ya nafaka na divai mupya.  8  Nitajilaza chini na kulala usingizi kwa amani,+Kwa maana wewe peke yako, Ee Yehova, unanifanya niishi katika usalama.+

Maelezo ya Chini

Tnn., “Unitengenezee nafasi kubwa katika.”
Ao “atamufanya mushikamanifu wake aonekane kuwa tofauti; atamutia pembeni mushikamanifu wake kwa ajili yake mwenyewe.”