Zaburi 37:1-40
Ya Daudi.
א [Aleph]
37 Usikasirike* kwa sababu ya waovuWala usisikilie wivu wakosaji.+
2 Watakauka haraka kama majani+Na kufifia kama majani ya mupya ya mubichi.
ב [Beth]
3 Umutegemee Yehova na utende mambo mema;+Kaa katika dunia,* na utende kwa uaminifu.+
4 Pata furaha nyingi sana* katika Yehova,Naye atakutimizia tamaa za moyo wako.
ג [Gimel]
5 Tia njia yako katika mukono wa* Yehova;+Umutegemee yeye, naye atatenda kwa ajili yako.+
6 Atafanya haki yako ingae kama mwangaza wa asubui sana,Na haki yako kama jua la katikati ya muchana.
ד [Daleth]
7 Nyamaza mbele ya Yehova+Na umungojee kwa matumaini.*
Usikasirishwe na mutuMwenye anafanikiwa katika kutimiza mipango yake ya mubaya.+
ה [He]
8 Acha hasira na uache kasirani kali;+Usikasirike na kuanza kutenda uovu.*
9 Kwa maana waovu wataharibiwa,+Lakini wale wenye kumutumainia Yehova watariti dunia.+
ו [Waw]
10 Kunabakia wakati kidogo tu, waovu hawatakuwa tena;+Utaangalia mahali walikuwa,Nao hawatakuwa pale.+
11 Lakini wapole watariti dunia,+Na watapata furaha nyingi sana katika wingi wa amani.+
ז [Zayin]
12 Mutu muovu anapanga mupango mubaya juu ya mwenye haki;+Anamusagia meno yake.
13 Lakini Yehova atamucheka,Kwa maana Anajua kwamba siku yake itakuja.+
ח [Heth]
14 Waovu wanachomoa panga zao na kukunja* pinde zaoIli kumuangusha chini mwenye kukandamizwa na maskini,Ili kuchinja wale wenye njia yao imenyooka.
15 Lakini upanga wao utatoboa moyo wao wenyewe;+Pinde zao zitavunjwa.
ט [Teth]
16 Kidogo yenye mwenye haki iko* nayo ni muzuriKuliko wingi wa vitu vyenye waovu wengi wako navyo.+
17 Kwa maana mikono ya waovu itavunjwa,Lakini Yehova atategemeza wenye haki.
י [Yod]
18 Yehova anajua mambo yenye watu wenye hawana lawama wanapambana nayo,*Na uriti wao utadumu milele.+
19 Hawatapatishwa haya wakati wa musiba;Wakati wa njaa watakuwa na chakula kingi.
כ [Kaph]
20 Lakini waovu wataangamia;+Maadui wa Yehova wataisha kama vile malisho yenye utukufu;Wataisha kama moshi.
ל [Lamed]
21 Muovu anakopa lakini halipe,Lakini mwenye haki ni mukarimu* na mwenye kutoa.+
22 Wale wenye kubarikiwa Naye watariti dunia,Lakini wale wenye kulaaniwa Naye wataharibiwa.+
מ [Mem]
23 Yehova anaongoza* hatua za mutu+Wakati Yeye anafurahia njia ya mutu huyo.+
24 Hata kama anaanguka, hatatupwa chini,+Kwa maana Yehova anamutegemeza kwa kumushika mukono.*+
נ [Nun]
25 Nilikuwa kijana na sasa nimezeeka,Lakini sijamuona mutu yeyote mwenye haki akiwa ameachwa,+Wala watoto wake wakitafuta mukate.*+
26 Sikuzote anakopesha bila kuomba faida,+Na watoto wake watapata baraka.
ס [Samekh]
27 Geuka na uache mambo ya mubaya na utende mambo ya muzuri,+Na utaishi milele.
28 Kwa maana Yehova anapenda haki,Na hataacha washikamanifu wake.+
ע [Ayin]
Watalindwa sikuzote;+Lakini wazao wa waovu wataharibiwa.+
29 Wenye haki watariti dunia,+Na wataishi milele juu yake.+
פ [Pe]
30 Kinywa cha mwenye haki kinajulisha hekima,*Na ulimi wake unaongea kuhusu haki.+
31 Sheria ya Mungu wake iko katika moyo wake;+Hatua zake hazitayumba-yumba.+
צ [Tsade]
32 Muovu anamuangalia mwenye haki,Akitafuta kumuua.
33 Lakini Yehova hatamuacha katika mukono wa mutu huyo+Wala hatamupata na hatia wakati atahukumiwa.+
ק [Qoph]
34 Tumainia Yehova na ufuate njia yake,Naye atakuinua ili uriti dunia.
Wakati waovu wataharibiwa,+ utaona jambo hilo.+
ר [Resh]
35 Nimemuona mutu mwenye hana huruma, muovuAkienea kama muti wenye majani mengi katika udongo wake wa asili.+
36 Lakini alikufa kwa kushitukia na hakukuwa tena;+Niliendelea kumutafuta, na hangeweza kupatikana.+
ש [Shin]
37 Angalia mutu mwenye hana lawama,*Na uendelee kumuangalia munyoofu,+Kwa maana wakati wenye kuja wa mutu huyo utakuwa wenye amani.+
38 Lakini wakosaji wote wataharibiwa;Wakati wenye kuja wa watu waovu utakomeshwa.+
ת [Taw]
39 Wokovu wa wenye haki unatoka kwa Yehova;+Yeye ndiye ngome yao wakati wa taabu.+
40 Yehova atawasaidia na kuwaokoa.+
Atawaokoa kutoka kwa waovu na kuwakomboa,Kwa sababu wanamukimbilia yeye.+
Maelezo ya Chini
^ Ao “Usiwake kasirani.”
^ Ao “inchi.”
^ Ao “Pata shangwe kubwa sana.”
^ Tnn., “Viringisha njia yako juu ya.”
^ Ao “kwa uvumilivu.”
^ Ao pengine, “Usikasirike, kwa maana kasirani itakuongoza tu kwenye mambo yenye kuumiza.”
^ Ao “kutia kamba kwenye.”
^ Ao “eko.”
^ Tnn., “siku za watu wenye hawana lawama.”
^ Ao “ni mwenye kuonyesha wema.”
^ Ao “anafanya imara.”
^ Ao “kwa mukono Wake.”
^ Ao “chakula.”
^ Ao “kinazungumuza hekima kwa sauti ya chini.”
^ Ao “mutu mwenye kushika uaminifu-mushikamanifu.”

