Zaburi 14:1-7
Kwa kiongozi. Ya Daudi.
14 Mupumbavu* anasema katika moyo wake:
“Hakuna Yehova.”+
Matendo yao yamepotoka, na shuguli zao zinachukiza;Hakuna mwenye kutenda mema.+
2 Lakini Yehova anaangalia wana wa binadamu akiwa mbinguniIli aone kama kuko mutu yeyote mwenye kuwa na ufahamu, kama kuko mutu yeyote mwenye kumutafuta Yehova.+
3 Wote wameenda pembeni;+Wote wamepotoka katika njia ileile.
Hakuna mwenye kutenda mema,Hakuna hata mumoja.
4 Je, hakuna hata mumoja kati ya wakosaji mwenye anaelewa?
Wanameza watu wangu kama vile wanakula mukate.
Hawamuitie Yehova.
5 Lakini watajaa woga mukubwa,+Kwa maana Yehova iko* pamoja na kizazi cha wenye haki.
6 Ninyi wakosaji munajaribu kuvuruga mipango ya mutu wa hali ya chini,Lakini Yehova ni kimbilio lake.+
7 Aa! kama tu wokovu wa Israeli ungetoka Sayuni!+
Wakati Yehova atakusanya tena watu wake wenye walikamatwa mateka,Yakobo ashangilie, Israeli afurahi.

