Zaburi 14:1-7

  • Maelezo kuhusu mupumbavu

    • “Hakuna Yehova” (1)

    • “Hakuna mwenye kutenda mema” (3)

Kwa kiongozi. Ya Daudi. 14  Mupumbavu* anasema katika moyo wake: “Hakuna Yehova.”+ Matendo yao yamepotoka, na shuguli zao zinachukiza;Hakuna mwenye kutenda mema.+  2  Lakini Yehova anaangalia wana wa binadamu akiwa mbinguniIli aone kama kuko mutu yeyote mwenye kuwa na ufahamu, kama kuko mutu yeyote mwenye kumutafuta Yehova.+  3  Wote wameenda pembeni;+Wote wamepotoka katika njia ileile. Hakuna mwenye kutenda mema,Hakuna hata mumoja.  4  Je, hakuna hata mumoja kati ya wakosaji mwenye anaelewa? Wanameza watu wangu kama vile wanakula mukate. Hawamuitie Yehova.  5  Lakini watajaa woga mukubwa,+Kwa maana Yehova iko* pamoja na kizazi cha wenye haki.  6  Ninyi wakosaji munajaribu kuvuruga mipango ya mutu wa hali ya chini,Lakini Yehova ni kimbilio lake.+  7  Aa! kama tu wokovu wa Israeli ungetoka Sayuni!+ Wakati Yehova atakusanya tena watu wake wenye walikamatwa mateka,Yakobo ashangilie, Israeli afurahi.

Maelezo ya Chini

Ao “Mwenye hana akili.”
Ao “eko.”