Zaburi 14:1-7

  • Maelezo kuhusu mupumbavu

    • “Hakuna Yehova” (1)

    • “Hakuna mwenye kutenda mema” (3)

Kwa kiongozi. Ya Daudi. 14  Mupumbavu* anasema katika moyo wake: “Hakuna Yehova.”+ Matendo yao yamepotoka, na shuguli zao zinachukiza; Hakuna mwenye kutenda mema.+   Lakini Yehova anaangalia wana wa binadamu akiwa mbinguni Ili aone kama kuko mutu yeyote mwenye kuwa na ufahamu, kama kuko mutu yeyote mwenye kumutafuta Yehova.+   Wote wameenda pembeni;+ Wote wamepotoka katika njia ileile. Hakuna mwenye kutenda mema, Hakuna hata mumoja.   Je, hakuna hata mumoja kati ya wakosaji mwenye anaelewa? Wanameza watu wangu kama vile wanakula mukate. Hawamuitie Yehova.   Lakini watajaa woga mukubwa,+ Kwa maana Yehova iko* pamoja na kizazi cha wenye haki.   Ninyi wakosaji munajaribu kuvuruga mipango ya mutu wa hali ya chini, Lakini Yehova ni kimbilio lake.+   Aa! kama tu wokovu wa Israeli ungetoka Sayuni!+ Wakati Yehova atakusanya tena watu wake wenye walikamatwa mateka, Yakobo ashangilie, Israeli afurahi.

Maelezo ya Chini

Ao “Mwenye hana akili.”
Ao “eko.”