Zaburi 108:1-13
Wimbo. Muziki wa Daudi.
108 Moyo wangu uko imara, Ee Mungu.
Nitaimba na kupiga muziki kwa nafsi yangu yote.*+
2 Amuka, Ee chombo cha kamba; na wewe pia, Ee kinubi.+
Nitaamusha mapambazuko.*
3 Nitakusifu kati ya vikundi vya watu, Ee Yehova,Na nitakuimbia sifa* kati ya mataifa.
4 Kwa maana upendo wako mushikamanifu ni mwingi, uko juu kama mbingu,+Na uaminifu wako, unafika mupaka kwenye anga.
5 Uinuliwe juu ya mbingu, Ee Mungu;Utukufu wako ukuwe juu ya dunia yote.+
6 Ili wapendwa wako waokolewe,Utuokoe kupitia mukono wako wa kuume na unijibu.+
7 Mungu amesema katika utakatifu wake:*
“Nitashangilia, nitatoa Shekemu+ kuwa uriti,Na nitapima Bonde* la Sukoti.+
8 Gileadi+ ni yangu, na Manase ni yangu,Na Efraimu ni kofia ya chuma* ya kichwa changu;+Yuda ni fimbo yangu ya kamanda.+
9 Moabu ni beseni yangu ya kunawia.+
Nitatupa kiatu changu juu ya Edomu.+
Nitapiga vigelegele vya ushindi juu ya Ufilisti.”+
10 Ni nani atanipeleka katika muji wenye ngome?
Ni nani ataniongoza mupaka Edomu?+
11 Je, haiko wewe, Ee Mungu, mwenye umetukataa,Mungu wetu, mwenye haende tena na majeshi yetu?+
12 Utusaidie katika taabu yetu,+Kwa maana wokovu kutoka kwa wanadamu hauna mafaa yoyote.+
13 Kwa musaada wa Mungu tutapata nguvu,+Na atakanyangia chini wapinzani wetu.+

