Zaburi 118:1-29
118 Mumushukuru Yehova, kwa maana yeye ni mwema;+Upendo wake mushikamanifu unadumu milele.
2 Israeli aseme sasa:
“Upendo wake mushikamanifu unadumu milele.”
3 Watu wa nyumba ya Haruni waseme sasa:
“Upendo wake mushikamanifu unadumu milele.”
4 Wale wenye kumuogopa Yehova waseme sasa:
“Upendo wake mushikamanifu unadumu milele.”
5 Nilimuitia Yah* katika taabu yangu;Yah akanijibu na kunipeleka mahali salama.*+
6 Yehova iko* upande wangu; sitaogopa.+
Mwanadamu anaweza kunifanya nini?+
7 Yehova iko* upande wangu akiwa musaidizi wangu;*+Nitaangalia kwa furaha kushindwa kwa wale wenye kunichukia.+
8 Ni muzuri kumukimbilia YehovaKuliko kutegemea wanadamu.+
9 Ni muzuri kumukimbilia YehovaKuliko kutegemea wakubwa.+
10 Mataifa yote yalinizunguka,Lakini katika jina la Yehova,Niliyafukuza.+
11 Yalinizunguka, ndiyo, yalinizunguka kabisa,Lakini katika jina la Yehova,Niliyafukuza.
12 Yalinizunguka kama nyuki,Lakini yalizimwa haraka kama moto kati ya miiba.
Katika jina la Yehova,Niliyafukuza.+
13 Nilisukumwa kwa nguvu* ili nianguke,Lakini Yehova alinisaidia.
14 Yah ni mahali pangu pa kujificha na nguvu zangu,Na amekuwa wokovu wangu.+
15 Sauti ya shangwe na wokovu*Iko katika mahema ya wenye haki.
Mukono wa kuume wa Yehova unaonyesha nguvu zake.+
16 Mukono wa kuume wa Yehova unajiinua;Mukono wa kuume wa Yehova unaonyesha nguvu zake.+
17 Sitakufa, hapana, nitaishi,Ili nitangaze kazi za Yah.+
18 Yah alinitia nizamu kwa ukali,+Lakini hakunitia katika mukono wa kifo.+
19 Munifungulie milango mikubwa ya haki;+Nitaingia ndani na kumusifu Yah.
20 Huu ni mulango mukubwa wa Yehova.
Wenye haki wataingia kupitia mulango huo.+
21 Nitakusifu, kwa maana ulinijibu+Na ukakuwa wokovu wangu.
22 Jiwe lenye wajenzi walikataaLimekuwa jiwe kubwa la pembe.*+
23 Hili limetoka kwa Yehova;+Ni la ajabu mbele ya macho yetu.+
24 Hii ndiyo siku yenye Yehova amefanya;Tutaifurahia na kuishangilia.
25 Yehova, utuokoe, tafazali, tunakulilia!
Yehova, utupatie ushindi, tafazali!
26 Amebarikiwa ule mwenye anakuja katika jina la Yehova;+Tunakubariki kutoka katika nyumba ya Yehova.
27 Yehova ni Mungu;Anatupatia mwangaza.+
Mujiunge na maandamano ya sikukuu mukiwa na matawi katika mikono,+Mupaka kwenye pembe za mazabahu.+
28 Wewe ni Mungu wangu, na nitakusifu;Mungu wangu, nitakutukuza.+
29 Mumushukuru Yehova,+ kwa maana yeye ni mwema;Upendo wake mushikamanifu unadumu milele.+

