Zaburi 48:1-14

  • Sayuni, muji wa Mufalme Mukubwa

    • Shangwe ya dunia yote (2)

    • Muchunguze muji na minara yake (11-13)

Wimbo. Muziki wa wana wa Kora.+ 48  Yehova ni mukubwa na anastahili kabisa kusifiwaKatika muji wa Mungu wetu, katika mulima wake mutakatifu.  2  Urefu wake unavutia, shangwe ya dunia yote,+Ni Mulima Sayuni wenye kuwa mbali sana kaskazini,Muji wa Mufalme Mukubwa.+  3  Katika minara yake yenye ngome,Mungu amejulisha kwamba yeye ni kimbilio salama.*+  4  Kwa maana angalia! wafalme wamekusanyika;*Wamesonga mbele pamoja.  5  Wakati waliona hilo, walishangaa. Walishikwa na wasiwasi na kukimbia kwa woga mukubwa.  6  Kutetemeka kuliwashika wakiwa kule,Uchungu kama wa mwanamuke mwenye kuzaa.  7  Kwa upepo wa mashariki unavunja-vunja mashua* za Tarshishi.  8  Mambo yenye tulisikia, tumejionea sasa sisi wenyeweKatika muji wa Yehova wa majeshi, katika muji wa Mungu wetu. Mungu ataufanya kuwa imara kabisa milele.+ (Sela)  9  Tunafikiri sana* juu ya upendo wako mushikamanifu, Ee Mungu,+Katika hekalu lako. 10  Kama jina lako, Ee Mungu, sifa yakoInafika mupaka kwenye miisho ya dunia.+ Mukono wako wa kuume umejaa haki.+ 11  Mulima Sayuni+ ushangilie,Miji ya Yuda ishangilie,* kwa sababu ya hukumu zako.+ 12  Mutembee kuzunguka Sayuni; muzunguke muji huo pande zote;Muhesabie minara yake.+ 13  Muweke mioyo yenu juu ya maboma yake.*+ Muchunguze minara yake yenye ngome,Ili muelezee vizazi vyenye kuja kuhusu muji huo. 14  Kwa maana Mungu huyu ni Mungu wetu+ milele na milele. Atatuongoza kwa umilele wote.*+

Maelezo ya Chini

Ao “mahali salama pa juu.”
Ao “wamekutana kwa mapatano.”
Ao “mashua za maji; bateaux.
Ao “Tunatafakari.”
Tnn., “Mabinti wa Yuda washangilie.”
Ao “kuta zake zenye ngome.”
Ao pengine, “mupaka wakati tutakufa.”