Zaburi 48:1-14
Wimbo. Muziki wa wana wa Kora.+
48 Yehova ni mukubwa na anastahili kabisa kusifiwaKatika muji wa Mungu wetu, katika mulima wake mutakatifu.
2 Urefu wake unavutia, shangwe ya dunia yote,+Ni Mulima Sayuni wenye kuwa mbali sana kaskazini,Muji wa Mufalme Mukubwa.+
3 Katika minara yake yenye ngome,Mungu amejulisha kwamba yeye ni kimbilio salama.*+
4 Kwa maana angalia! wafalme wamekusanyika;*Wamesonga mbele pamoja.
5 Wakati waliona hilo, walishangaa.
Walishikwa na wasiwasi na kukimbia kwa woga mukubwa.
6 Kutetemeka kuliwashika wakiwa kule,Uchungu kama wa mwanamuke mwenye kuzaa.
7 Kwa upepo wa mashariki unavunja-vunja mashua* za Tarshishi.
8 Mambo yenye tulisikia, tumejionea sasa sisi wenyeweKatika muji wa Yehova wa majeshi, katika muji wa Mungu wetu.
Mungu ataufanya kuwa imara kabisa milele.+ (Sela)
9 Tunafikiri sana* juu ya upendo wako mushikamanifu, Ee Mungu,+Katika hekalu lako.
10 Kama jina lako, Ee Mungu, sifa yakoInafika mupaka kwenye miisho ya dunia.+
Mukono wako wa kuume umejaa haki.+
11 Mulima Sayuni+ ushangilie,Miji ya Yuda ishangilie,* kwa sababu ya hukumu zako.+
12 Mutembee kuzunguka Sayuni; muzunguke muji huo pande zote;Muhesabie minara yake.+
13 Muweke mioyo yenu juu ya maboma yake.*+
Muchunguze minara yake yenye ngome,Ili muelezee vizazi vyenye kuja kuhusu muji huo.
14 Kwa maana Mungu huyu ni Mungu wetu+ milele na milele.
Atatuongoza kwa umilele wote.*+

