Zaburi 127:1-5

  • Bila Mungu, kila kitu ni bure

    • “Kama Yehova hajenge nyumba” (1)

    • Watoto ni zawabu kutoka kwa Mungu (3)

Wimbo wa Safari za Kupanda. Wa Sulemani. 127  Kama Yehova hajenge nyumba, Wale wenye kuijenga wanafanya kazi ya nguvu ya bure.+ Kama Yehova halinde muji,+ Mulinzi anakesha bure.   Ni bure kwamba munaamuka asubui sana, Kwamba munachelewa kulala, Kwamba munafanya kazi ya jasho ili kupata chakula, Kwa maana yeye anaandalia wale wenye anapenda na anawapatia usingizi.+   Angalia! Wana* ni uriti kutoka kwa Yehova;+ Uzao wa tumbo la uzazi ni zawabu.+   Kama mishale katika mukono wa mwanaume mwenye nguvu, Ni vile pia wana wa ujana wa mutu.+   Mwenye furaha ni mwanaume mwenye anawajaza katika mufuko wake wa mishale.+ Hawatapatishwa haya, Kwa maana watazungumuza na maadui katika mulango mukubwa wa muji.

Maelezo ya Chini

Ao “Watoto.”