Zaburi 127:1-5
Wimbo wa Safari za Kupanda. Wa Sulemani.
127 Kama Yehova hajenge nyumba,Wale wenye kuijenga wanafanya kazi ya nguvu ya bure.+
Kama Yehova halinde muji,+Mulinzi anakesha bure.
2 Ni bure kwamba munaamuka asubui sana,Kwamba munachelewa kulala,Kwamba munafanya kazi ya jasho ili kupata chakula,Kwa maana yeye anaandalia wale wenye anapenda na anawapatia usingizi.+
3 Angalia! Wana* ni uriti kutoka kwa Yehova;+Uzao wa tumbo la uzazi ni zawabu.+
4 Kama mishale katika mukono wa mwanaume mwenye nguvu,Ni vile pia wana wa ujana wa mutu.+
5 Mwenye furaha ni mwanaume mwenye anawajaza katika mufuko wake wa mishale.+
Hawatapatishwa haya,Kwa maana watazungumuza na maadui katika mulango mukubwa wa muji.
Maelezo ya Chini
^ Ao “Watoto.”

