Zaburi 127:1-5

  • Bila Mungu, kila kitu ni bure

    • “Kama Yehova hajenge nyumba” (1)

    • Watoto ni zawabu kutoka kwa Mungu (3)

Wimbo wa Safari za Kupanda. Wa Sulemani. 127  Kama Yehova hajenge nyumba,Wale wenye kuijenga wanafanya kazi ya nguvu ya bure.+ Kama Yehova halinde muji,+Mulinzi anakesha bure.  2  Ni bure kwamba munaamuka asubui sana,Kwamba munachelewa kulala,Kwamba munafanya kazi ya jasho ili kupata chakula,Kwa maana yeye anaandalia wale wenye anapenda na anawapatia usingizi.+  3  Angalia! Wana* ni uriti kutoka kwa Yehova;+Uzao wa tumbo la uzazi ni zawabu.+  4  Kama mishale katika mukono wa mwanaume mwenye nguvu,Ni vile pia wana wa ujana wa mutu.+  5  Mwenye furaha ni mwanaume mwenye anawajaza katika mufuko wake wa mishale.+ Hawatapatishwa haya,Kwa maana watazungumuza na maadui katika mulango mukubwa wa muji.

Maelezo ya Chini

Ao “Watoto.”