Zaburi 79:1-13

  • Sala wakati mataifa yalivamia watu wa Mungu

    • ‘Tuko kitu cha kulaumiwa’ (4)

    • ‘Utusaidie kwa ajili ya jina lako’ (9)

    • “Lipa majirani wetu mara saba” (12)

Muziki wa Asafu.+ 79  Ee Mungu, mataifa yamevamia uriti wako;+Yamechafua hekalu lako takatifu;+Yamegeuza Yerusalemu kuwa rundo la mabomoko.+  2  Yamepatia ndege wa mbinguni maiti za watumishi wako kuwa chakulaNa miili ya washikamanifu wako yameipatia wanyama wa pori wa dunia.+  3  Yamemwanga damu yao kama maji kotekote Yerusalemu,Na hakuna mwenye alibakia ili kuwazika.+  4  Tumekuwa kitu cha kulaumiwa na majirani wetu;+Wale wenye kutuzunguka wanatuzihaki na kutuchekelea.  5  Ee Yehova, utaendelea kukasirika sana mupaka wakati gani? Milele?+ Kasirani yako kali itaendelea kuwaka kama vile moto mupaka wakati gani?+  6  Mwanga kasirani yako kali juu ya mataifa yenye hayakujueNa juu ya falme zenye haziitie jina lako.+  7  Kwa maana wamemumeza YakoboNa wamefanya inchi yake ikuwe ukiwa.+  8  Usituombe tutoe hesabu kwa sababu ya makosa ya mababu zetu.+ Utuonyeshe haraka rehema yako,+Kwa maana tumeshushwa chini sana.  9  Utusaidie, Ee Mungu wa wokovu wetu,+Kwa ajili ya jina lako lenye utukufu;Utuokoe na usamehe* zambi zetu kwa ajili ya jina lako.+ 10  Sababu gani mataifa yaseme: “Mungu wao iko* wapi?”+ Acha ijulikane kati ya mataifa mbele ya macho yetuKwamba damu yenye ilimwangwa ya watumishi wako imelipiziwa kisasi.+ 11  Sikia kilio cha maumivu cha mufungwa.+ Tumia nguvu zako kubwa* ili kulinda* wale wenye walihukumiwa kifo.*+ 12  Lipa majirani wetu mara saba (7)+Kwa sababu ya zihaka zenye walikufanyia, Ee Yehova.+ 13  Kisha sisi, watu wako na kundi la malisho yako,+Tutakushukuru milele;Na tutatangaza sifa yako kizazi kwa kizazi.+

Maelezo ya Chini

Tnn., “ufunike.”
Ao “eko.”
Tnn., “mukono wako.”
Ao pengine, “kuweka huru.”
Tnn., “wana wa kifo.”