Zaburi 79:1-13
Muziki wa Asafu.+
79 Ee Mungu, mataifa yamevamia uriti wako;+
Yamechafua hekalu lako takatifu;+
Yamegeuza Yerusalemu kuwa rundo la mabomoko.+
2 Yamepatia ndege wa mbinguni maiti za watumishi wako kuwa chakula
Na miili ya washikamanifu wako yameipatia wanyama wa pori wa dunia.+
3 Yamemwanga damu yao kama maji kotekote Yerusalemu,
Na hakuna mwenye alibakia ili kuwazika.+
4 Tumekuwa kitu cha kulaumiwa na majirani wetu;+
Wale wenye kutuzunguka wanatuzihaki na kutuchekelea.
5 Ee Yehova, utaendelea kukasirika sana mupaka wakati gani? Milele?+
Kasirani yako kali itaendelea kuwaka kama vile moto mupaka wakati gani?+
6 Mwanga kasirani yako kali juu ya mataifa yenye hayakujue
Na juu ya falme zenye haziitie jina lako.+
7 Kwa maana wamemumeza Yakobo
Na wamefanya inchi yake ikuwe ukiwa.+
8 Usituombe tutoe hesabu kwa sababu ya makosa ya mababu zetu.+
Utuonyeshe haraka rehema yako,+
Kwa maana tumeshushwa chini sana.
9 Utusaidie, Ee Mungu wa wokovu wetu,+
Kwa ajili ya jina lako lenye utukufu;
Utuokoe na usamehe* zambi zetu kwa ajili ya jina lako.+
10 Sababu gani mataifa yaseme: “Mungu wao iko* wapi?”+
Acha ijulikane kati ya mataifa mbele ya macho yetu
Kwamba damu yenye ilimwangwa ya watumishi wako imelipiziwa kisasi.+
11 Sikia kilio cha maumivu cha mufungwa.+
Tumia nguvu zako kubwa* ili kulinda* wale wenye walihukumiwa kifo.*+
12 Lipa majirani wetu mara saba (7)+
Kwa sababu ya zihaka zenye walikufanyia, Ee Yehova.+
13 Kisha sisi, watu wako na kundi la malisho yako,+
Tutakushukuru milele;
Na tutatangaza sifa yako kizazi kwa kizazi.+
Maelezo ya Chini
^ Tnn., “ufunike.”
^ Ao “eko.”
^ Tnn., “mukono wako.”
^ Ao pengine, “kuweka huru.”
^ Tnn., “wana wa kifo.”