Zaburi 79:1-13

  • Sala wakati mataifa yalivamia watu wa Mungu

    • ‘Tuko kitu cha kulaumiwa’ (4)

    • ‘Utusaidie kwa ajili ya jina lako’ (9)

    • “Lipa majirani wetu mara saba” (12)

Muziki wa Asafu.+ 79  Ee Mungu, mataifa yamevamia uriti wako;+ Yamechafua hekalu lako takatifu;+ Yamegeuza Yerusalemu kuwa rundo la mabomoko.+   Yamepatia ndege wa mbinguni maiti za watumishi wako kuwa chakula Na miili ya washikamanifu wako yameipatia wanyama wa pori wa dunia.+   Yamemwanga damu yao kama maji kotekote Yerusalemu, Na hakuna mwenye alibakia ili kuwazika.+   Tumekuwa kitu cha kulaumiwa na majirani wetu;+ Wale wenye kutuzunguka wanatuzihaki na kutuchekelea.   Ee Yehova, utaendelea kukasirika sana mupaka wakati gani? Milele?+ Kasirani yako kali itaendelea kuwaka kama vile moto mupaka wakati gani?+   Mwanga kasirani yako kali juu ya mataifa yenye hayakujue Na juu ya falme zenye haziitie jina lako.+   Kwa maana wamemumeza Yakobo Na wamefanya inchi yake ikuwe ukiwa.+   Usituombe tutoe hesabu kwa sababu ya makosa ya mababu zetu.+ Utuonyeshe haraka rehema yako,+ Kwa maana tumeshushwa chini sana.   Utusaidie, Ee Mungu wa wokovu wetu,+ Kwa ajili ya jina lako lenye utukufu; Utuokoe na usamehe* zambi zetu kwa ajili ya jina lako.+ 10  Sababu gani mataifa yaseme: “Mungu wao iko* wapi?”+ Acha ijulikane kati ya mataifa mbele ya macho yetu Kwamba damu yenye ilimwangwa ya watumishi wako imelipiziwa kisasi.+ 11  Sikia kilio cha maumivu cha mufungwa.+ Tumia nguvu zako kubwa* ili kulinda* wale wenye walihukumiwa kifo.*+ 12  Lipa majirani wetu mara saba (7)+ Kwa sababu ya zihaka zenye walikufanyia, Ee Yehova.+ 13  Kisha sisi, watu wako na kundi la malisho yako,+ Tutakushukuru milele; Na tutatangaza sifa yako kizazi kwa kizazi.+

Maelezo ya Chini

Tnn., “ufunike.”
Ao “eko.”
Tnn., “mukono wako.”
Ao pengine, “kuweka huru.”
Tnn., “wana wa kifo.”