Zaburi 1:1-6

  • Tofauti kati ya njia mbili inaonyeshwa

    • Kusoma sheria ya Mungu kunaleta furaha (2)

    • Wenye haki wako kama muti wenye kuzaa matunda kwa wingi (3)

    • Waovu wako kama maganda ya mbegu yenye kupeperushwa mbali (4)

1  Mwenye furaha ni mutu mwenye hatembee kulingana na shauri la waovuNa hasimame katika njia ya watenda-zambi+Naye hakae katika kiti cha wenye kuzihaki.+  2  Lakini anapendezwa na sheria ya Yehova,+Na anasoma sheria Yake kwa sauti ya chini* muchana na usiku.+  3  Atakuwa kama muti wenye kupandwa pembeni ya mito midogo ya maji,Muti wenye unazaa matunda katika wakati wake,Na majani yake hayakauke. Na kila jambo lenye anafanya litafanikiwa.+  4  Waovu hawako vile;Wako kama maganda ya mbegu yenye kupeperushwa mbali na upepo.  5  Ndiyo sababu waovu hawataendelea kusimama katika hukumu;+Wala watenda-zambi hawataendelea kusimama katika mukusanyiko wa wenye haki.+  6  Kwa maana Yehova anajua njia ya wenye haki,+Lakini njia ya waovu itaangamia.+

Maelezo ya Chini

Ao “anatafakari juu ya sheria Yake; anafikiri sana juu ya sheria Yake.”