Zaburi 123:1-4
Wimbo wa Safari za Kupanda.
123 Ninainua macho yangu kukuelekea wewe,+
Wewe mwenye kukaa ukiwa mufalme mbinguni.
2 Kama vile macho ya watumishi yanaangalia mukono wa bwana wao,
Na macho ya mutumishi mwanamuke yanaangalia mukono wa bimukubwa wake,
Ni vile macho yetu yanamuangalia Yehova Mungu wetu+
Mupaka wakati atatuonyesha wema.+
3 Utuonyeshe wema, Ee Yehova, utuonyeshe wema,
Kwa maana tumezarauliwa kwa ukamili.+
4 Tumechekelewa kwa ukamili na* watu wenye kujitumainia
Na tumezarauliwa na watu wenye kiburi.
Maelezo ya Chini
^ Ao “Nafsi yetu imechokeshwa sababu ya kuchekelewa sana na.”