Zaburi 123:1-4

  • Kumutegemea Yehova ili kupata rehema

    • ‘Kama vile watumishi, tunamuangalia Yehova’ (2)

    • ‘Tumezarauliwa kwa ukamili’ (3)

Wimbo wa Safari za Kupanda. 123  Ninainua macho yangu kukuelekea wewe,+ Wewe mwenye kukaa ukiwa mufalme mbinguni.   Kama vile macho ya watumishi yanaangalia mukono wa bwana wao, Na macho ya mutumishi mwanamuke yanaangalia mukono wa bimukubwa wake, Ni vile macho yetu yanamuangalia Yehova Mungu wetu+ Mupaka wakati atatuonyesha wema.+   Utuonyeshe wema, Ee Yehova, utuonyeshe wema, Kwa maana tumezarauliwa kwa ukamili.+   Tumechekelewa kwa ukamili na* watu wenye kujitumainia Na tumezarauliwa na watu wenye kiburi.

Maelezo ya Chini

Ao “Nafsi yetu imechokeshwa sababu ya kuchekelewa sana na.”