Zaburi 123:1-4

  • Kumutegemea Yehova ili kupata rehema

    • ‘Kama vile watumishi, tunamuangalia Yehova’ (2)

    • ‘Tumezarauliwa kwa ukamili’ (3)

Wimbo wa Safari za Kupanda. 123  Ninainua macho yangu kukuelekea wewe,+Wewe mwenye kukaa ukiwa mufalme mbinguni.  2  Kama vile macho ya watumishi yanaangalia mukono wa bwana wao,Na macho ya mutumishi mwanamuke yanaangalia mukono wa bimukubwa wake,Ni vile macho yetu yanamuangalia Yehova Mungu wetu+Mupaka wakati atatuonyesha wema.+  3  Utuonyeshe wema, Ee Yehova, utuonyeshe wema,Kwa maana tumezarauliwa kwa ukamili.+  4  Tumechekelewa kwa ukamili na* watu wenye kujitumainiaNa tumezarauliwa na watu wenye kiburi.

Maelezo ya Chini

Ao “Nafsi yetu imechokeshwa sababu ya kuchekelewa sana na.”