Zaburi 28:1-9
-
Sala ya muandikaji wa zaburi inasikiwa
-
‘Yehova ni nguvu zangu na ngao yangu’ (7)
-
Ya Daudi.
28 Ninaendelea kukuita, Ee Yehova Mwamba wangu;+Usikuwe kama kiziwi kwangu.
Kama unaninyamazia,Nitakuwa kama wale wenye kushuka katika shimo.*+
2 Sikia vilio vyangu wakati ninakulilia unisaidieWakati ninainua mikono yangu kuelekea chumba cha ndani zaidi cha patakatifu pako.+
3 Usinikokote pamoja na waovu, pamoja na wale wenye kuzoea kutenda mambo yenye kuumiza,+Wale wenye kuongea na mwanadamu mwenzao maneno ya amani wakati uovu uko katika mioyo yao.+
4 Uwalipe kulingana na matendo yao,+Kulingana na mazoea yao maovu.
Uwalipe kulingana na kazi ya mikono yao,Kulingana na mambo yenye wametenda.+
5 Kwa maana hawakazie uangalifu utendaji wa Yehova,+Wala kazi ya mikono yake.+
Atawabomoa na hatawajenga.
6 Yehova asifiwe,Kwa maana amesikia vilio vyangu vya kuomba musaada.
7 Yehova ni nguvu zangu+ na ngao yangu;+Moyo wangu unamutegemea yeye.+
Nimepokea musaada wake, na moyo wangu unashangilia,Kwa hiyo nitamusifu kwa wimbo wangu.
8 Yehova ni nguvu kwa watu wake;Yeye ni ngome, anamuletea mutiwa-mafuta wake wokovu mukubwa.+
9 Uokoe watu wako, na ubariki uriti wako.+
Uwachunge na uwabebe katika mikono yako milele.+
Maelezo ya Chini
^ Ao “kaburi.”