Zaburi 28:1-9

  • Sala ya muandikaji wa zaburi inasikiwa

    • ‘Yehova ni nguvu zangu na ngao yangu’ (7)

Ya Daudi. 28  Ninaendelea kukuita, Ee Yehova Mwamba wangu;+Usikuwe kama kiziwi kwangu. Kama unaninyamazia,Nitakuwa kama wale wenye kushuka katika shimo.*+  2  Sikia vilio vyangu wakati ninakulilia unisaidieWakati ninainua mikono yangu kuelekea chumba cha ndani zaidi cha patakatifu pako.+  3  Usinikokote pamoja na waovu, pamoja na wale wenye kuzoea kutenda mambo yenye kuumiza,+Wale wenye kuongea na mwanadamu mwenzao maneno ya amani wakati uovu uko katika mioyo yao.+  4  Uwalipe kulingana na matendo yao,+Kulingana na mazoea yao maovu. Uwalipe kulingana na kazi ya mikono yao,Kulingana na mambo yenye wametenda.+  5  Kwa maana hawakazie uangalifu utendaji wa Yehova,+Wala kazi ya mikono yake.+ Atawabomoa na hatawajenga.  6  Yehova asifiwe,Kwa maana amesikia vilio vyangu vya kuomba musaada.  7  Yehova ni nguvu zangu+ na ngao yangu;+Moyo wangu unamutegemea yeye.+ Nimepokea musaada wake, na moyo wangu unashangilia,Kwa hiyo nitamusifu kwa wimbo wangu.  8  Yehova ni nguvu kwa watu wake;Yeye ni ngome, anamuletea mutiwa-mafuta wake wokovu mukubwa.+  9  Uokoe watu wako, na ubariki uriti wako.+ Uwachunge na uwabebe katika mikono yako milele.+

Maelezo ya Chini

Ao “kaburi.”