Zaburi 136:1-26

  • Upendo mushikamanifu wa Yehova unadumu milele

    • Mbingu na dunia zilifanywa kwa ufundi (5, 6)

    • Farao alikufa katika Bahari Nyekundu (15)

    • Mungu anakumbuka wenye kushuka moyo (23)

    • Anapatia chakula kila kiumbe chenye uzima (25)

136  Mumushukuru Yehova, kwa maana ni mwema;+Upendo wake mushikamanifu unadumu milele.+  2  Mumushukuru Mungu wa miungu,+Kwa maana upendo wake mushikamanifu unadumu milele.  3  Mumushukuru Bwana wa mabwana,Kwa maana upendo wake mushikamanifu unadumu milele.  4  Yeye peke yake ndiye anafanya mambo makubwa ya ajabu,+Kwa maana upendo wake mushikamanifu unadumu milele.+  5  Alifanya mbingu kwa ufundi,*+Kwa maana upendo wake mushikamanifu unadumu milele.  6  Alitandika dunia juu ya maji,+Kwa maana upendo wake mushikamanifu unadumu milele.  7  Alifanya vitu vikubwa vya kutoa mwangaza,+Kwa maana upendo wake mushikamanifu unadumu milele,  8  Jua ili litawale muchana,+Kwa maana upendo wake mushikamanifu unadumu milele,  9  Mwezi na nyota ili vitawale usiku,+Kwa maana upendo wake mushikamanifu unadumu milele. 10  Alipiga na kuua muzaliwa wa kwanza wa Misri,+Kwa maana upendo wake mushikamanifu unadumu milele. 11  Alitosha Israeli katikati yao,+Kwa maana upendo wake mushikamanifu unadumu milele, 12  Kwa mukono wenye nguvu+ na mukono wenye kunyooshwa,Kwa maana upendo wake mushikamanifu unadumu milele. 13  Aligawa Bahari Nyekundu katika sehemu mbili,*+Kwa maana upendo wake mushikamanifu unadumu milele. 14  Alifanya Israeli apite katikati ya ile bahari,+Kwa maana upendo wake mushikamanifu unadumu milele. 15  Alimukunguta Farao na jeshi lake ndani ya Bahari Nyekundu,+Kwa maana upendo wake mushikamanifu unadumu milele. 16  Alipitisha watu wake katika jangwa,+Kwa maana upendo wake mushikamanifu unadumu milele. 17  Alipiga na kuua wafalme wakubwa,+Kwa maana upendo wake mushikamanifu unadumu milele. 18  Aliua wafalme wenye nguvu,Kwa maana upendo wake mushikamanifu unadumu milele. 19  Sihoni+ mufalme wa Waamori,Kwa maana upendo wake mushikamanifu unadumu milele, 20  Na Ogu+ mufalme wa Bashani,Kwa maana upendo wake mushikamanifu unadumu milele. 21  Alitoa inchi yao kuwa uriti,+Kwa maana upendo wake mushikamanifu unadumu milele. 22  Uriti kwa Israeli mutumishi wake,Kwa maana upendo wake mushikamanifu unadumu milele. 23  Alitukumbuka wakati tulikuwa katika hali ya chini,+Kwa maana upendo wake mushikamanifu unadumu milele.+ 24  Aliendelea kutuokoa kutoka kwa wapinzani wetu,+Kwa maana upendo wake mushikamanifu unadumu milele. 25  Anapatia chakula kila kiumbe chenye uzima,*+Kwa maana upendo wake mushikamanifu unadumu milele. 26  Mumushukuru Mungu wa mbinguni,Kwa maana upendo wake mushikamanifu unadumu milele.

Maelezo ya Chini

Ao “kwa uelewaji.”
Tnn., “vipande-vipande.”
Tnn., “miili yote.”