Zaburi 136:1-26
136 Mumushukuru Yehova, kwa maana ni mwema;+Upendo wake mushikamanifu unadumu milele.+
2 Mumushukuru Mungu wa miungu,+Kwa maana upendo wake mushikamanifu unadumu milele.
3 Mumushukuru Bwana wa mabwana,Kwa maana upendo wake mushikamanifu unadumu milele.
4 Yeye peke yake ndiye anafanya mambo makubwa ya ajabu,+Kwa maana upendo wake mushikamanifu unadumu milele.+
5 Alifanya mbingu kwa ufundi,*+Kwa maana upendo wake mushikamanifu unadumu milele.
6 Alitandika dunia juu ya maji,+Kwa maana upendo wake mushikamanifu unadumu milele.
7 Alifanya vitu vikubwa vya kutoa mwangaza,+Kwa maana upendo wake mushikamanifu unadumu milele,
8 Jua ili litawale muchana,+Kwa maana upendo wake mushikamanifu unadumu milele,
9 Mwezi na nyota ili vitawale usiku,+Kwa maana upendo wake mushikamanifu unadumu milele.
10 Alipiga na kuua muzaliwa wa kwanza wa Misri,+Kwa maana upendo wake mushikamanifu unadumu milele.
11 Alitosha Israeli katikati yao,+Kwa maana upendo wake mushikamanifu unadumu milele,
12 Kwa mukono wenye nguvu+ na mukono wenye kunyooshwa,Kwa maana upendo wake mushikamanifu unadumu milele.
13 Aligawa Bahari Nyekundu katika sehemu mbili,*+Kwa maana upendo wake mushikamanifu unadumu milele.
14 Alifanya Israeli apite katikati ya ile bahari,+Kwa maana upendo wake mushikamanifu unadumu milele.
15 Alimukunguta Farao na jeshi lake ndani ya Bahari Nyekundu,+Kwa maana upendo wake mushikamanifu unadumu milele.
16 Alipitisha watu wake katika jangwa,+Kwa maana upendo wake mushikamanifu unadumu milele.
17 Alipiga na kuua wafalme wakubwa,+Kwa maana upendo wake mushikamanifu unadumu milele.
18 Aliua wafalme wenye nguvu,Kwa maana upendo wake mushikamanifu unadumu milele.
19 Sihoni+ mufalme wa Waamori,Kwa maana upendo wake mushikamanifu unadumu milele,
20 Na Ogu+ mufalme wa Bashani,Kwa maana upendo wake mushikamanifu unadumu milele.
21 Alitoa inchi yao kuwa uriti,+Kwa maana upendo wake mushikamanifu unadumu milele.
22 Uriti kwa Israeli mutumishi wake,Kwa maana upendo wake mushikamanifu unadumu milele.
23 Alitukumbuka wakati tulikuwa katika hali ya chini,+Kwa maana upendo wake mushikamanifu unadumu milele.+
24 Aliendelea kutuokoa kutoka kwa wapinzani wetu,+Kwa maana upendo wake mushikamanifu unadumu milele.
25 Anapatia chakula kila kiumbe chenye uzima,*+Kwa maana upendo wake mushikamanifu unadumu milele.
26 Mumushukuru Mungu wa mbinguni,Kwa maana upendo wake mushikamanifu unadumu milele.

