Zaburi 140:1-13

  • Yehova ni Mwokozi mwenye nguvu

    • Waovu wako kama nyoka (3)

    • Watu wenye jeuri wataanguka (11)

Kwa kiongozi. Muziki wa Daudi. 140  Uniokoe, Ee Yehova, kutoka kwa watu waovu;Unilinde kutoka kwa watu wenye jeuri,+  2  Wale wenye kufanya mipango ya uovu katika mioyo yao+Na kuchochea ugomvi muchana wote.  3  Wananoa ulimi wao kama ule wa nyoka;+Sumu ya nyoka-vipiri iko nyuma ya midomo yao.+ (Sela)  4  Unilinde, Ee Yehova, kutokana na mikono ya waovu;+Unilinde kutokana na watu wenye jeuri,Wale wenye kufanya mupango wa kunifanya nijikwae.  5  Wenye majivuno wanaficha mutego ili uninase;Kwa kamba wanatandika wavu* pembeni ya njia.+ Wanatega mitego ya kuninasa.+ (Sela)  6  Ninamuambia Yehova: “Wewe ni Mungu wangu. Sikiliza, Ee Yehova, vilio vyangu vya kuomba musaada.”+  7  Ee Yehova Bwana Mwenye Mamlaka Makubwa Zaidi, Mwokozi wangu mwenye nguvu,Wewe unalinda kichwa changu katika siku ya vita.+  8  Ee Yehova, usitimize tamaa za waovu. Usiruhusu mipango yao mibaya ifanikiwe, ili wasijiinue.+ (Sela)  9  Vichwa vya wale wenye kunizungukaVifunikwe na uovu wenye kusemwa na midomo yao.+ 10  Makaa yenye kuwaka yawanyeshee.+ Watupwe katika moto,Ndani ya mashimo ya murefu,*+ wasisimame tena hata siku moja. 11  Muchongezi asipate makao juu ya dunia.*+ Uovu ufuatilie watu wenye jeuri na uwapige na kuwaua. 12  Ninajua kwamba Yehova atatetea watu wa hali ya chiniNa kupatia maskini haki.+ 13  Hakika wenye haki watashukuru jina lako;Watu wanyoofu watakaa mbele ya uso wako.*+

Maelezo ya Chini

Ao “makila.”
Ao “Ndani ya mashimo yenye maji.”
Ao “katika inchi.”
Ao “katika kuwapo kwako.”