Ona video zinazopatikana

Ukumbusho wa Kifo ya Yesu

Siku ya Yenga, Tarehe 24, Mwezi wa 3, 2024

Mara moya kila mwaka, Mashahidi wa Yehova wanafanyaka ukumbusho wa kifo ya Yesu. Wanafuata amri yenye Yesu alitoa wakati alisema hivi: “Muendelee kufanya hivi kwa kunikumbuka mimi.”​​—Luka 22:19.

Tunakualika ku hii tukio.

Maulizo Yenye Watu Wanaulizaka Mara Mingi

Ile programu itafanya saa ngapi?

Itafanya karibu saa moya.

Itafanyika wapi?

Uzungumuze na Mashahidi wa Yehova wa fasi kwenye unaishi.

Itaomba kulipa juu ya kuingia?

Hapana.

Wataniomba sadaka?

Hapana. Mashahidi wa Yehova hawaombake sadaka ku mikutano yao.

Inaomba kuvala manguo ya namna gani?

Ku ile mukutano haiombe kuvala manguo ya aina fulani tu. Lakini Mashahidi wa Yehova wanajikazaka kufuata shauri ya Biblia ya kuvala kwa kiasi na kwa heshima. (1 Timoteo 2:9) Haiombe uvale manguo ya bei sana ao ya heshima sana.

Ukumbusho utafanywa namna gani?

Ile mukutano itaanza na kumalizika na wimbo na sala. Sala itatolewa na muzee mwenye ni Shahidi wa Yehova. Sehemu kubwa ya ile mukutano ni hotuba yenye itaonyesha juu ya nini Yesu alikufa na kile tunaweza kufanya juu tupate faida ya mambo yenye Mungu na Yesu walitufanyia.