Tunakualika kwa Furaha

Ibada Safi

Mukusanyiko wa Eneo wa Mashahidi wa Yehova wa 2025

Tafuta  Mukusanyiko  Wenye  Utafanyika  Karibu  na  Kwenye  Unaishi

Kuingia ni bure Habatakulomba sadaka

Mambo Makubwa ya Mukusanyiko

Siku ya Tano: Kupitia mavideo mbalimbali, utaona namna maisha ilikuwa fasi kwenye Yesu aliishi na kwenye alihubiri.

Siku ya Posho: Utaona namna sehemu ya kwanza ya utumishi wa Yesu ilitimiza maunabii yenye ilitabiriwa kumepita mamia ya miaka.

Siku ya Yenga: Mu hotuba “Unaabudu Kile Unajua?” utaona juu ya nini ni jambo ya maana kuhangaikia mambo yenye unaamini na namna ya kupata kweli.

Drama

Habari Njema Juu ya Yesu: Epizode ya 2 na ya 3

Wakati Yesu alibatizwa alifikia kuwa Masiya, ao Kristo. Mu miezi yenye kufuata, alijaribiwa na Ibilisi, alianza kutafuta benye balipaswa kuwa banafunzi yake, na alifanya miujiza yake ya kwanza. Utaona ile mambo na mambo ingine mu maepizode yenye itaonyeshwa kila siku ya mukusanyiko.

Fungula jw.org juu ya kupata programu yote ya mukusanyiko na uangalie video zenye kufuata:

Mikusanyiko Yetu Inafanyikaka Namna Gani?

Ona vile mukusanyiko wa Mashahidi wa Yehova unafanyikaka.

Mukusanyiko wa Eneo wa Mashahidi wa Yehova wa 2025: “Ibada Safi”

Ona mambo yenye tutajifunza ku mukusanyiko wa hii mwaka.

Kifupi ya Drama: Habari Njema Juu ya Yesu

Tangu tu mwanzo wa utumishi wake, Yesu Kristo alipingwa na batu, Ibilisi, na mashetani wake. Yesu alimuacha Mungu?