ULIZO LA 7
Biblia Ilitabiri Nini Juu Ya Siku Zetu?
“Taifa litasimama kupigana na taifa na ufalme kupigana na ufalme . . . Mambo hayo yote ni mwanzo wa maumivu ya taabu.”
“Manabii wengi wa uongo watatokea na kupotosha watu wengi; na kwa sababu ya kuongezeka kwa uvunjaji wa sheria, upendo wa watu wengi utapoa.”
“Wakati mutasikia juu ya vita na habari za vita, musiogope; mambo hayo lazima yatokee, lakini ule mwisho bado.”
“Kutakuwa matetemeko makubwa ya inchi, na mahali pamoja kisha pengine kutakuwa upungufu wa chakula na magonjwa ya kuambukiza; na kutakuwa mambo yenye kuogopesha na alama kubwa kutoka mbinguni.”
“Katika siku za mwisho kutakuwa nyakati za hatari zenye kuwa ngumu kuvumilia. Kwa maana watu watakuwa wenye kujipenda wenyewe, wenye kupenda feza, wenye kujisifu, wenye kujivuna, wenye kumutukana Mungu, wenye hawatii wazazi, wenye hawana shukrani, wenye hawana ushikamanifu, wenye hawana upendo wa asili, wenye hawataki makubaliano yoyote, wachongezi, wenye hawajizuie, wakali, wenye hawapendi wema, wasaliti, wenye vichwa vigumu, wenye kujivuna kwa kiburi, wenye kupenda raha kuliko kumupenda Mungu, wenye kwa inje wanaonekana kuwa na ushikamanifu kwa Mungu lakini wanakana nguvu za ushikamanifu huo.”