Zaburi 6:1-10
Kwa kiongozi; iimbwe kwa vyombo vya kamba vyenye vimepatanishwa na sauti ya Sheminiti.* Muziki wa Daudi.
6 Ee Yehova, usinikaripie katika hasira yako,Na usinirekebishe katika kasirani yako kali.+
2 Unionyeshe wema,* Ee Yehova, kwa maana ninakuwa muzaifu.
Uniponyeshe, Ee Yehova,+ kwa maana mifupa yangu inatetemeka.
3 Ndiyo, ninavurugika* sana;+Na ninakuuliza, Ee Yehova—itakuwa mupaka wakati gani?+
4 Rudia, Ee Yehova, na uniokoe;*+Uniokoe kwa ajili ya upendo wako mushikamanifu.+
5 Kwa maana hakuna kukutaja* katika kifo;Katika Kaburi,* ni nani atakusifu?+
6 Nimechoka kwa sababu ya kilio changu cha maumivu;+Usiku wote ninalowanisha kitanda changu kwa machozi;*Kiti changu ninakifanya kijae kilio.+
7 Jicho langu limekuwa zaifu kwa sababu ya huzuni yangu,+Limefifia* kwa sababu ya wale wote wenye kunisumbua.
8 Mutoke mbele yangu, ninyi wote wenye kutenda uovu,Kwa maana Yehova atasikia sauti ya kilio changu.+
9 Yehova atasikia ombi langu la kuomba rehema;+Yehova atakubali sala yangu.
10 Maadui wangu wote watapatishwa haya na kufazaishwa;Watarudia nyuma katika haya ya kushitukia.+
Maelezo ya Chini
^ Angalia Maana ya Maneno.
^ Ao “rehema.”
^ Ao “nafsi yangu inavurugika.”
^ Ao “uokoe nafsi yangu.”
^ Ao “kukukumbuka.”
^ Ao “Sheoli,” ni kusema, kaburi la wanadamu wote. Angalia Maana ya Maneno.
^ Tnn., “ninafanya kitanda changu kiogelee.”
^ Ao “Limezeeka.”

