Zaburi 92:1-15
Muziki. Wimbo wa siku ya Sabato.
92 Ni muzuri kumushukuru Yehova+Na kuimbia jina lako sifa,* Ee Mwenye Kuwa Juu Zaidi,
2 Kutangaza upendo wako mushikamanifu+ asubuiNa uaminifu wako nyakati za usiku,
3 Kwa chombo cha kamba kumi (10) na kwa udi,Kwa mulio mutamu wa kinubi.+
4 Kwa maana umenifanya nishangilie, Ee Yehova, kwa sababu ya matendo yako;Kwa sababu ya kazi za mikono yako ninapiga vigelegele vya shangwe.
5 Kazi zako ni kubwa sana, Ee Yehova!+
Mawazo yako ni mazito sana!+
6 Mutu yeyote mwenye hana akili hawezi kuyajua;Na hakuna mupumbavu mwenye anaweza kuelewa hili:+
7 Wakati waovu wanachipuka kama magugu*Na wakati wakosaji wote wanasitawi,Ni ili waharibiwe milele.+
8 Lakini wewe umeinuliwa milele, Ee Yehova.
9 Kwa kweli, angalia kwa furaha kushindwa kwa maadui wako, Ee Yehova,Angalia namna maadui wako wataangamia;Wakosaji wote watasambazwa.+
10 Lakini utainua nguvu zangu kama za* ngombe-dume wa pori;Nitapakaa ngozi yangu mafuta ya mupya.+
11 Macho yangu yataangalia kwa furaha kushindwa kwa maadui wangu;+Masikio yangu yatasikia kuhusu kuanguka kwa watu waovu wenye kunishambulia.
12 Lakini wenye haki watasitawi kama muti wa mutendeNa watakuwa wakubwa kama mwerezi katika Lebanoni.+
13 Wamepandwa katika nyumba ya Yehova;Wanasitawi katika viwanja vya Mungu wetu.+
14 Hata wakati wa uzee* wataendelea kusitawi;+Wataendelea kuwa na nguvu* na kuwa wabichi,+
15 Wakitangaza kwamba Yehova ni munyoofu.
Yeye ni Mwamba wangu,+ mwenye ndani yake hakuna ukosefu wa haki.

