Zaburi 105:1-45
-
Matendo ya uaminifu ya Yehova kuelekea watu wake
105 Mumushukuru Yehova,+ muitie jina lake,Mujulishe matendo yake kati ya vikundi vya watu!+
2 Mumuimbie, mumuimbie sifa,*Mufikiri sana* juu ya kazi zake zote za ajabu.+
3 Mujisifu juu ya jina lake takatifu.+
Mioyo ya wale wenye kumutafuta Yehova ishangilie.+
4 Mumutafute Yehova+ na nguvu zake.
Mutafute uso* wake bila kuacha.
5 Mukumbuke kazi za ajabu zenye amefanya,Miujiza yake na hukumu zenye ametangaza,+
6 Ninyi uzao wa* Abrahamu mutumishi wake,+Ninyi wana wa Yakobo, wachaguliwa wake.+
7 Yeye ni Yehova Mungu wetu.+
Hukumu zake ziko katika dunia yote.+
8 Anakumbuka agano lake milele,+Ahadi yenye alitoa,* mupaka vizazi elfu,+
9 Agano lenye alifanya pamoja na Abrahamu,+Na kiapo chenye alimuapia Isaka,+
10 Chenye aliweka kuwa amri kwa YakoboNa kuwa agano la kudumu kwa Israeli,
11 Akisema, “Nitakupatia inchi ya Kanaani+Kuwa uriti wenu wenye muligawiwa.”+
12 Ilikuwa vile wakati walikuwa hesabu kidogo,+Ndiyo, kidogo sana, na walikuwa wageni katika inchi.+
13 Walitembea-tembea kutoka taifa moja mupaka taifa lingine,Kutoka ufalme mumoja mupaka kikundi kingine cha watu.+
14 Hakumuruhusu mutu yeyote awakandamize,+Lakini kwa sababu yao alikaripia wafalme,+
15 Kwa kusema, “Musiguse watiwa-mafuta wangu,Na musitendee manabii wangu jambo lolote la mubaya.”+
16 Alileta njaa katika inchi;+Aliondoa akiba yao ya mikate.*
17 Alituma mutu mumoja awatangulieMwenye aliuzishwa ili kuwa mutumwa, Yosefu.+
18 Walifunga* miguu yake kwa pingu,+Shingo yake ilitiwa katika vyuma;*
19 Mupaka wakati neno lake lilitimia,+Neno la Yehova ndilo lilimusafisha.
20 Mufalme alituma watu wamufungue,+Mutawala wa vikundi vya watu alimuweka huru.
21 Akamufanya kuwa bwana wa nyumba yake,Mutawala juu ya mali zake zote,+
22 Ili akuwe na mamlaka juu ya* wakubwa wake namna alipenda*Na ili afundishe wazee wake hekima.+
23 Kisha Israeli akaingia Misri,+Na Yakobo akakaa akiwa mugeni katika inchi ya Hamu.
24 Mungu alifanya watu wake waongezeke sana;+Aliwafanya wakuwe na nguvu kuliko wapinzani wao,+
25 Aliruhusu mioyo yao ibadilike ili wachukie watu wake,Ili wafanye mupango mubaya juu ya watumishi wake.+
26 Alimutuma Musa mutumishi wake,+Na Haruni,+ mwenye alikuwa amechagua.
27 Walifanya alama zake kati yao,Miujiza yake katika inchi ya Hamu.+
28 Alituma giza na inchi ikakuwa giza;+Hawakuasi maneno yake.
29 Alibadilisha maji yao kuwa damuNa kuua samaki wao.+
30 Inchi yao ikajaa vyura,+Hata katika vyumba vya kifalme.
31 Aliagiza mainzi wavamieNa imbu katika maeneo yao yote.+
32 Alibadilisha mvua yao kuwa mvua ya majiweNa kutuma umeme wa radi* katika inchi yao.+
33 Alipiga mizabibu yao na miti yao ya tiniNa kuvunja-vunja miti ya eneo lao.
34 Alisema nzige wavamie,Nzige wadogo wenye hawakukuwa na hesabu.+
35 Walikula mimea yote katika inchi,Na walimeza mazao ya udongo.
36 Kisha akapiga na kuua kila muzaliwa wa kwanza katika inchi yao,+Mwanzo wa nguvu zao za uzazi.
37 Alipeleka watu wake inje wakiwa na feza na zahabu;+Na hakuna mutu yeyote kati ya makabila yake mwenye alijikwaa.
38 Misri ilishangilia wakati waliondoka,Kwa maana woga mukubwa wa Israeli* ulikuwa umewaangukia.+
39 Alitandika wingu ili liwafunike+
Na moto ili utoe mwangaza wakati wa usiku.+
40 Waliomba, naye akaleta kware;+Aliendelea kuwashibisha mukate kutoka mbinguni.+
41 Alifungua mwamba, na maji yakatiririka;+Maji hayo yalitiririka katika jangwa kama muto.+
42 Kwa maana alikumbuka ahadi takatifu yenye alimupatia Abrahamu mutumishi wake.+
43 Kwa hiyo akatosha watu wake wakishangilia,+Alitosha wachaguliwa wake kwa vigelegele vya shangwe.
44 Aliwapatia inchi za mataifa;+Waliriti vitu vyenye vikundi vingine vya watu vilikuwa vimetumika sana ili kuvitengeneza,+
45 Ili watii maagizo yake+Na kushika sheria zake.
Mumusifu Yah!*
Maelezo ya Chini
^ Ao pengine, “Museme.”
^ Ao “mumupigie muziki.”
^ Ao “kuwapo.”
^ Ao “wazao wa.” Tnn., “mbegu ya.”
^ Tnn., “Neno lenye aliamuru.”
^ Tnn., “Alivunja kila fimbo ya mukate.” Inawezekana ni fimbo zenye zilikuwa zinatumiwa ili kuwekea mikate.
^ Tnn., “Walitesa.”
^ Ao “Nafsi yake iliingia katika chuma.”
^ Tnn., “Ili afunge.”
^ Ao “kwa njia yenye kupendeza nafsi yake.”
^ Ao “miali ya moto.”
^ Tnn., “wao.”
^ Ao “Haleluya!” “Yah” ni kifupi cha jina Yehova.