Zaburi 34:1-22

  • Yehova anaokoa watumishi wake

    • “Tutukuze jina lake pamoja” (3)

    • Malaika wa Yehova analinda (7)

    • “Muonje na muone kwamba Yehova ni mwema” (8)

    • ‘Hakuna mumoja kati ya mifupa yake wenye ulivunjwa’ (20)

Ya Daudi, wakati alijifanya mwenda-wazimu+ mbele yaAbimeleki, mwenye alimufukuza,na akaenda zake. א [Aleph] 34  Nitamusifu Yehova nyakati zote;Sifa yake itakuwa kwenye midomo yangu kila wakati. ב [Beth]  2  Nitajisifu* katika Yehova;+Wapole watasikia na kushangilia. ג [Gimel]  3  Mumutukuze Yehova pamoja na mimi;+Tutukuze jina lake pamoja. ד [Daleth]  4  Nilimuuliza Yehova, na akanijibu.+ Aliniokoa katika mambo yote yenye kuniogopesha.+ ה [He]  5  Wale wenye walimuangalia walingaa;Nyuso zao hazingeweza kupatishwa haya. ז [Zayin]  6  Mutu huyu wa hali ya chini aliita, na Yehova akasikia. Alimuokoa katika taabu zake zote.+ ח [Heth]  7  Malaika wa Yehova anapiga kambi pande zote kuzunguka wale wenye kumuogopa Yeye,+Na anawaokoa.+ ט [Teth]  8  Muonje na muone kwamba Yehova ni mwema;+Mwenye furaha ni mutu mwenye anamukimbilia. י [Yod]  9  Mumuogope Yehova, ninyi wote watakatifu wake,Kwa maana wale wenye kumuogopa hawakose kitu.+ כ [Kaph] 10  Hata wana-simba wenye nguvu* wamelemewa na njaa,Lakini wale wenye kumutafuta Yehova hawatakosa kitu kizuri.+ ל [Lamed] 11  Mukuje, wana wangu, munisikilize;Nitawafundisha kumuogopa Yehova.+ מ [Mem] 12  Ni nani kati yenu anapenda uzimaNa angependa kuona siku nyingi za muzuri?+ נ [Nun] 13  Basi linda ulimi wako kutokana na ubaya,+Midomo yako isiseme udanganyifu.+ ס [Samekh] 14  Geuka na uache mambo ya mubaya na utende mambo ya muzuri;+Tafuta amani na uifuatie.+ ע [Ayin] 15  Macho ya Yehova yako juu ya wenye haki,+Na masikio yake yanasikiliza kilio chao cha kuomba musaada.+ פ [Pe] 16  Lakini uso wa Yehova unapinga wale wenye kutenda mambo ya mubaya,Ili afute kumbukumbu lao lote katika dunia.+ צ [Tsade] 17  Walilia kwa sauti kubwa, na Yehova akasikia;+Aliwaokoa katika taabu zao zote.+ ק [Qoph] 18  Yehova iko* karibu na wale wenye kuvunjika moyo;+Anaokoa wale wenye kupondwa roho.*+ ר [Resh] 19  Magumu ya mwenye haki ni mengi,*+Lakini Yehova anamuokoa katika magumu hayo yote.+ ש [Shin] 20  Analinda mifupa yake yote;Hakuna mumoja kati ya mifupa yake wenye umevunjwa.+ ת [Taw] 21  Musiba utamuua muovu;Wale wenye kumuchukia mwenye haki watapatikana na hatia. 22  Yehova anakomboa uzima wa* watumishi wake;Hakuna mutu yeyote kati ya wenye kumukimbilia mwenye atapatikana na hatia.+

Maelezo ya Chini

Ao “Nafsi yangu itajisifu.”
Ao “wana-simba wenye manyoya ya murefu kwenye shingo.”
Ao “eko.”
Ao “wenye kuvunjika moyo.”
Ao “Misiba ya mwenye haki ni mingi.”
Ao “nafsi ya.”