Zaburi 34:1-22
Ya Daudi, wakati alijifanya mwenda-wazimu+ mbele yaAbimeleki, mwenye alimufukuza,na akaenda zake.
א [Aleph]
34 Nitamusifu Yehova nyakati zote;Sifa yake itakuwa kwenye midomo yangu kila wakati.
ב [Beth]
2 Nitajisifu* katika Yehova;+Wapole watasikia na kushangilia.
ג [Gimel]
3 Mumutukuze Yehova pamoja na mimi;+Tutukuze jina lake pamoja.
ד [Daleth]
4 Nilimuuliza Yehova, na akanijibu.+
Aliniokoa katika mambo yote yenye kuniogopesha.+
ה [He]
5 Wale wenye walimuangalia walingaa;Nyuso zao hazingeweza kupatishwa haya.
ז [Zayin]
6 Mutu huyu wa hali ya chini aliita, na Yehova akasikia.
Alimuokoa katika taabu zake zote.+
ח [Heth]
7 Malaika wa Yehova anapiga kambi pande zote kuzunguka wale wenye kumuogopa Yeye,+Na anawaokoa.+
ט [Teth]
8 Muonje na muone kwamba Yehova ni mwema;+Mwenye furaha ni mutu mwenye anamukimbilia.
י [Yod]
9 Mumuogope Yehova, ninyi wote watakatifu wake,Kwa maana wale wenye kumuogopa hawakose kitu.+
כ [Kaph]
10 Hata wana-simba wenye nguvu* wamelemewa na njaa,Lakini wale wenye kumutafuta Yehova hawatakosa kitu kizuri.+
ל [Lamed]
11 Mukuje, wana wangu, munisikilize;Nitawafundisha kumuogopa Yehova.+
מ [Mem]
12 Ni nani kati yenu anapenda uzimaNa angependa kuona siku nyingi za muzuri?+
נ [Nun]
13 Basi linda ulimi wako kutokana na ubaya,+Midomo yako isiseme udanganyifu.+
ס [Samekh]
14 Geuka na uache mambo ya mubaya na utende mambo ya muzuri;+Tafuta amani na uifuatie.+
ע [Ayin]
15 Macho ya Yehova yako juu ya wenye haki,+Na masikio yake yanasikiliza kilio chao cha kuomba musaada.+
פ [Pe]
16 Lakini uso wa Yehova unapinga wale wenye kutenda mambo ya mubaya,Ili afute kumbukumbu lao lote katika dunia.+
צ [Tsade]
17 Walilia kwa sauti kubwa, na Yehova akasikia;+Aliwaokoa katika taabu zao zote.+
ק [Qoph]
18 Yehova iko* karibu na wale wenye kuvunjika moyo;+Anaokoa wale wenye kupondwa roho.*+
ר [Resh]
19 Magumu ya mwenye haki ni mengi,*+Lakini Yehova anamuokoa katika magumu hayo yote.+
ש [Shin]
20 Analinda mifupa yake yote;Hakuna mumoja kati ya mifupa yake wenye umevunjwa.+
ת [Taw]
21 Musiba utamuua muovu;Wale wenye kumuchukia mwenye haki watapatikana na hatia.
22 Yehova anakomboa uzima wa* watumishi wake;Hakuna mutu yeyote kati ya wenye kumukimbilia mwenye atapatikana na hatia.+
Maelezo ya Chini
^ Ao “Nafsi yangu itajisifu.”
^ Ao “wana-simba wenye manyoya ya murefu kwenye shingo.”
^ Ao “eko.”
^ Ao “wenye kuvunjika moyo.”
^ Ao “Misiba ya mwenye haki ni mingi.”
^ Ao “nafsi ya.”