Zaburi 111:1-10

  • Mumusifu Yehova kwa sababu ya kazi zake kubwa

    • Jina la Mungu ni takatifu na lenye kuogopesha sana (9)

    • Kumuogopa Yehova ni hekima (10)

111  Mumusifu Yah!*+ א [Aleph] Nitamusifu Yehova kwa moyo wangu wote+ב [Beth]Katika kikundi chenye kimekusanyika cha watu wanyoofu na katika kutaniko. ג [Gimel]  2  Kazi za Yehova ni kubwa;+ד [Daleth]Wale wote wenye kupendezwa nazo wanajifunza kuhusu kazi hizo.+ ה [He]  3  Kazi zake ni zenye utukufu na ni zenye kupendeza sana,ו [Waw]Na haki yake inadumu milele.+ ז [Zayin]  4  Anafanya kazi zake za ajabu zikumbukwe.+ ח [Heth] Yehova ni mwenye huruma* na mwenye rehema.+ ט [Teth]  5  Anapatia chakula wale wenye kumuogopa.+ י [Yod] Anakumbuka agano lake milele.+ כ [Kaph]  6  Amefunulia watu wake matendo yake yenye nguvuל [Lamed]Kwa kuwapatia uriti wa mataifa.+ מ [Mem]  7  Kazi za mikono yake ni kweli na haki;+נ [Nun]Maagizo yake yote yanategemeka.+ ס [Samekh]  8  Yanategemeka* sikuzote, sasa na milele;ע [Ayin]Yamefanywa katika kweli na haki.+ פ [Pe]  9  Amepatia watu wake ukombozi.+ צ [Tsade] Aliamuru kwamba agano lake linapaswa kudumu milele. ק [Qoph] Jina lake ni takatifu na ni lenye kuogopesha sana.+ ר [Resh] 10  Kumuogopa Yehova ni mwanzo wa hekima.+ ש [Sin] Wale wote wenye kushika maagizo yake wanaonyesha ufahamu muzuri.+ ת [Taw] Sifa yake inadumu milele.

Maelezo ya Chini

Ao “Haleluya!” “Yah” ni kifupi cha jina Yehova.
Ao “neema.”
Ao “Yako na musingi muzuri.”