Zaburi 83:1-18
Wimbo. Muziki wa Asafu.+
83 Ee Mungu, usinyamaze;+Usikae kimya* wala kutulia, Ee Mungu.
2 Kwa maana, angalia! maadui wako wanafanya fujo;+Wale wenye kukuchukia wanatenda kwa kiburi.*
3 Kwa udanganyifu wanafanya mupango kwa uficho ili kushambulia watu wako;Wanafanya mupango ili kushambulia watu wako wenye unapenda sana.*
4 Wanasema: “Mukuje, tuwaharibu wakiwa taifa,+Ili jina la Israeli lisikumbukwe tena.”
5 Wanafanya mupango mubaya kwa umoja;*Wamefanya mapatano* ili kukushambulia+—
6 Mahema ya Edomu na Waishmaeli, Moabu+ na Wahagri,+
7 Gebali na Amoni+ na Amaleki,Ufilisti+ pamoja na wakaaji wa Tiro.+
8 Ashuru+ pia imejiunga nao;Wanategemeza* wana wa Loti.+ (Sela)
9 Uwatendee kama vile ulitendea Midiani,+Kama vile ulitendea Sisera na Yabini kwenye muto mudogo wa* Kishoni.+
10 Waliharibiwa kule En-dori;+Wakakuwa mbolea juu ya udongo.
11 Fanya watu wao wenye vyeo wakuwe kama Orebu na Zeebu+Na wakubwa* wao kama Zeba na Zalmuna,+
12 Kwa maana walisema: “Turiti inchi kwenye Mungu anakaa.”
13 Ee Mungu wangu, uwafanye wakuwe kama muchongoma wenye kupeperushwa,*+Kama majani yenye kukauka yenye yanapeperushwa huku na huku na upepo.
14 Kama moto wenye unateketeza pori,Kama mwali wa moto wenye unaunguza milima,+
15 Uwafuatilie basi kwa zoruba yako yenye upepo mukali+Na kuwaogopesha sana kupitia upepo wako wa zoruba.+
16 Funika* nyuso zao haya,Ili watafute jina lako, Ee Yehova.
17 Wapatishwe haya na kuogopeshwa sana milele;Wafezeheshwe na kuangamia;
18 Wajue kwamba wewe, mwenye jina lako ni Yehova,+Wewe peke yako ndiye Mwenye Kuwa Juu Zaidi, juu ya dunia yote.+

