Zaburi 137:1-9

  • Pembeni ya mito ya Babiloni

    • Nyimbo za Sayuni hazikuimbwa (3, 4)

    • Babiloni itaharibiwa (8)

137  Pembeni ya mito ya Babiloni,+ ni pale tulikaa. Tulilia wakati tulikumbuka Sayuni.+  2  Juu ya miti ya mierebi yenye ilikuwa katikati yake,*Tulitundika vinubi vyetu.+  3  Kwa maana kule, wenye walitukamata walituomba tuwaimbie wimbo,+Wale wenye kutuchekelea walitaka tuwafurahishe: “Mutuimbie moja ya nyimbo za Sayuni.”  4  Namna gani tunaweza kuimba wimbo wa YehovaKwenye udongo wa kigeni?  5  Kama ninakusahau, Ee Yerusalemu,Acha mukono wangu wa kuume ukuwe musahaulifu.*+  6  Ulimi wangu ushikamane na kaakaa* languKama sikukumbuke,Kama sitie Yerusalemu juu yaSababu zangu kubwa zaidi za kushangilia.+  7  Kumbuka, Ee Yehova,Mambo yenye Waedomu walisema siku yenye Yerusalemu ilianguka: “Muibomoe! Muibomoe mupaka kwenye misingi yake!”+  8  Ee binti ya Babiloni, mwenye kuwa karibu kuharibiwa,+Mwenye furaha ni ule mwenye atakupatia zawabuMambo yenye ulitutendea.+  9  Mwenye furaha ni ule mwenye atakamata watoto wakoNa kuwapiga-piga juu ya miamba.+

Maelezo ya Chini

Ni kusema, katikati ya Babiloni.
Ao pengine, “ukauke.”
Kaakaa ni sehemu ya juu ndani ya kinywa.