Zaburi 137:1-9
137 Pembeni ya mito ya Babiloni,+ ni pale tulikaa.
Tulilia wakati tulikumbuka Sayuni.+
2 Juu ya miti ya mierebi yenye ilikuwa katikati yake,*Tulitundika vinubi vyetu.+
3 Kwa maana kule, wenye walitukamata walituomba tuwaimbie wimbo,+Wale wenye kutuchekelea walitaka tuwafurahishe:
“Mutuimbie moja ya nyimbo za Sayuni.”
4 Namna gani tunaweza kuimba wimbo wa YehovaKwenye udongo wa kigeni?
5 Kama ninakusahau, Ee Yerusalemu,Acha mukono wangu wa kuume ukuwe musahaulifu.*+
6 Ulimi wangu ushikamane na kaakaa* languKama sikukumbuke,Kama sitie Yerusalemu juu yaSababu zangu kubwa zaidi za kushangilia.+
7 Kumbuka, Ee Yehova,Mambo yenye Waedomu walisema siku yenye Yerusalemu ilianguka:
“Muibomoe! Muibomoe mupaka kwenye misingi yake!”+
8 Ee binti ya Babiloni, mwenye kuwa karibu kuharibiwa,+Mwenye furaha ni ule mwenye atakupatia zawabuMambo yenye ulitutendea.+
9 Mwenye furaha ni ule mwenye atakamata watoto wakoNa kuwapiga-piga juu ya miamba.+

