Zaburi 137:1-9

  • Pembeni ya mito ya Babiloni

    • Nyimbo za Sayuni hazikuimbwa (3, 4)

    • Babiloni itaharibiwa (8)

137  Pembeni ya mito ya Babiloni,+ ni pale tulikaa. Tulilia wakati tulikumbuka Sayuni.+   Juu ya miti ya mierebi yenye ilikuwa katikati yake,* Tulitundika vinubi vyetu.+   Kwa maana kule, wenye walitukamata walituomba tuwaimbie wimbo,+ Wale wenye kutuchekelea walitaka tuwafurahishe: “Mutuimbie moja ya nyimbo za Sayuni.”   Namna gani tunaweza kuimba wimbo wa Yehova Kwenye udongo wa kigeni?   Kama ninakusahau, Ee Yerusalemu, Acha mukono wangu wa kuume ukuwe musahaulifu.*+   Ulimi wangu ushikamane na kaakaa* langu Kama sikukumbuke, Kama sitie Yerusalemu juu ya Sababu zangu kubwa zaidi za kushangilia.+   Kumbuka, Ee Yehova, Mambo yenye Waedomu walisema siku yenye Yerusalemu ilianguka: “Muibomoe! Muibomoe mupaka kwenye misingi yake!”+   Ee binti ya Babiloni, mwenye kuwa karibu kuharibiwa,+ Mwenye furaha ni ule mwenye atakupatia zawabu Mambo yenye ulitutendea.+   Mwenye furaha ni ule mwenye atakamata watoto wako Na kuwapiga-piga juu ya miamba.+

Maelezo ya Chini

Ni kusema, katikati ya Babiloni.
Ao pengine, “ukauke.”
Kaakaa ni sehemu ya juu ndani ya kinywa.