Zaburi 137:1-9
137 Pembeni ya mito ya Babiloni,+ ni pale tulikaa.
Tulilia wakati tulikumbuka Sayuni.+
2 Juu ya miti ya mierebi yenye ilikuwa katikati yake,*
Tulitundika vinubi vyetu.+
3 Kwa maana kule, wenye walitukamata walituomba tuwaimbie wimbo,+
Wale wenye kutuchekelea walitaka tuwafurahishe:
“Mutuimbie moja ya nyimbo za Sayuni.”
4 Namna gani tunaweza kuimba wimbo wa Yehova
Kwenye udongo wa kigeni?
5 Kama ninakusahau, Ee Yerusalemu,
Acha mukono wangu wa kuume ukuwe musahaulifu.*+
6 Ulimi wangu ushikamane na kaakaa* langu
Kama sikukumbuke,
Kama sitie Yerusalemu juu ya
Sababu zangu kubwa zaidi za kushangilia.+
7 Kumbuka, Ee Yehova,
Mambo yenye Waedomu walisema siku yenye Yerusalemu ilianguka:
“Muibomoe! Muibomoe mupaka kwenye misingi yake!”+
8 Ee binti ya Babiloni, mwenye kuwa karibu kuharibiwa,+
Mwenye furaha ni ule mwenye atakupatia zawabu
Mambo yenye ulitutendea.+
9 Mwenye furaha ni ule mwenye atakamata watoto wako
Na kuwapiga-piga juu ya miamba.+
Maelezo ya Chini
^ Ni kusema, katikati ya Babiloni.
^ Ao pengine, “ukauke.”
^ Kaakaa ni sehemu ya juu ndani ya kinywa.