Zaburi 59:1-17
Kwa kiongozi; imepatanishwa na “Usiharibu.” Ya Daudi. Miktamu.* Wakati Sauli alituma watu wachunguze nyumba ya Daudi* ili wamuue.+
59 Uniokoe kutoka kwa maadui wangu, Ee Mungu wangu;+Unilinde kutoka kwa wale wenye kusimama ili kunishambulia.+
2 Uniokoe kutoka kwa wale wenye kutenda uovu,Na uniokoe kutoka kwa watu wenye jeuri.*
3 Angalia! Wananivizia;*+Wanaume wenye nguvu wananishambuliaLakini haiko kwa sababu nimeasi ao kutenda zambi,+ Ee Yehova.
4 Hata kama sikutenda kosa lolote, wanakimbia na kujitayarisha ili kushambulia.
Simama wakati ninakuita na uone.
5 Kwa maana wewe, Ee Yehova Mungu wa majeshi, ni Mungu wa Israeli.+
Amuka ili ukazie uangalifu wako mataifa yote.
Usionyeshe rehema wasaliti wowote wenye nia mubaya.+ (Sela)
6 Wanarudia kila mangaribi;+Wananguruma* kama imbwa+ na kuzunguka wakivizia-vizia katika muji.+
7 Angalia kile kinamwangika* kutoka katika kinywa chao;Midomo yao ni kama panga,+Kwa maana wanasema: “Ni nani anasikiliza?”+
8 Lakini wewe, Ee Yehova, utawacheka;+Utachekelea mataifa yote.+
9 Ee Nguvu zangu, nitaendelea kukungojea;+Kwa maana Mungu ni kimbilio langu salama.*+
10 Mungu mwenye ananitendea kwa upendo mushikamanifu atanisaidia;+Mungu ataniwezesha niangalie kwa furaha kushindwa kwa maadui wangu.+
11 Usiwaue, ili watu wangu wasisahau.
Kwa nguvu zako uwafanye watange-tange;Uwaangushe, Ee Yehova, ngao yetu.+
12 Kwa sababu ya zambi ya kinywa chao, neno la midomo yao,Acha kiburi chao kiwanase,+Kwa sababu ya laana na udanganyifu wenye wanasema.
13 Uwamalize kwa kasirani yako kali;+Uwamalize, ili wasikuwe tena;Uwafanye wajue kwamba Mungu anatawala katika Yakobo na mupaka kwenye miisho ya dunia.+ (Sela)
14 Acha warudie mangaribi;Acha wangurume* kama imbwa na kuzunguka wakivizia-vizia katika muji.+
15 Acha watange-tange wakitafuta chakula;+Usiwaruhusu washibe wala kupata makao.
16 Lakini mimi, nitaimba kuhusu nguvu zako;+Asubui nitatangaza kwa shangwe kuhusu upendo wako mushikamanifu.
Kwa maana wewe ni kimbilio langu salama+Na mahali pangu pa kukimbilia wakati niko katika taabu.+
17 Ee Nguvu zangu, nitakuimbia sifa,*+Kwa maana Mungu ni kimbilio langu salama, Mungu mwenye kunionyesha upendo mushikamanifu.+

