Zaburi 33:1-22

  • Sifa kwa Muumbaji

    • “Mumuimbie wimbo mupya” (3)

    • Yehova anaumba kupitia neno lake na roho yake (6)

    • Taifa la Yehova lenye furaha (12)

    • Jicho la Yehova lenye kulinda (18)

33  Mupige vigelegele vya shangwe, kwa sababu ya Yehova, ninyi wenye haki.+ Ni jambo lenye kufaa kwa wanyoofu kumusifu yeye.   Mumushukuru Yehova kwa kinubi; Mumuimbie sifa* kwa chombo cha kamba kumi (10).   Mumuimbie wimbo mupya;+ Mupige kamba kwa ufundi, pamoja na vigelegele vya shangwe.   Kwa maana neno la Yehova limenyooka,+ Na kila jambo lenye anafanya linategemeka.   Anapenda uadilifu* na haki.+ Dunia imejaa upendo mushikamanifu wa Yehova.+   Kwa neno la Yehova mbingu zilifanywa,+ Na kwa roho* ya kinywa chake kila kitu chenye kuwa katika mbingu kilifanywa.*   Anakusanya maji ya bahari kama vile ukuta wa maji;+ Anatia maji yenye mawimbi makubwa katika madepo.   Dunia yote imuogope Yehova.+ Wakaaji wa inchi yenye kuzaa wamuogope sana.   Kwa maana alisema, na ikakuwa vile;+ Aliamuru, na ikasimama imara.+ 10  Yehova amevuruga mipango mibaya ya* mataifa;+ Amevunja mipango* ya vikundi vya watu.+ 11  Lakini maamuzi ya Yehova yatasimama* milele;+ Mawazo ya moyo wake ni ya kizazi kwa kizazi. 12  Lenye furaha ni taifa lenye Mungu wake ni Yehova,+ Watu wenye amechagua kuwa mali yake mwenyewe.+ 13  Yehova anaangalia chini akiwa mbinguni; Anaona wana wote wa binadamu.+ 14  Akiwa katika makao yake, Anakazia macho wakaaji wa dunia. 15  Yeye ndiye anaumba mioyo ya wote; Anachunguza kazi zao zote.+ 16  Hakuna mufalme mwenye anaokolewa kupitia jeshi kubwa;+ Mutu mwenye nguvu haokolewe kupitia nguvu zake nyingi.+ 17  Farasi ni tumaini la uongo la wokovu;*+ Nguvu zake nyingi hazihakikishe kuponyoka. 18  Angalia! Jicho la Yehova linalinda wale wenye kumuogopa,+ Wale wenye kungojea upendo wake mushikamanifu, 19  Ili awaokoe* katika kifo Na kulinda uzima wao wakati wa njaa.+ 20  Tunamungojea* Yehova. Yeye ni musaidizi wetu na ngao yetu.+ 21  Mioyo yetu inashangilia katika yeye, Kwa maana tunategemea jina lake takatifu.+ 22  Upendo wako mushikamanifu ukae juu yetu, Ee Yehova,+ Wakati tunaendelea kukungojea.+

Maelezo ya Chini

Ao “Mumupigie muziki.”
Angalia Maana ya Maneno.
Ao “jeshi lote la mbinguni lilifanywa.”
Ao “pumuzi.”
Ao “mawazo.”
Ao “shauri la.”
Ao “shauri la Yehova litasimama.”
Ao “la ushindi.”
Ao “aokoe nafsi yao.”
Ao “Nafsi yetu inamungojea.”