Zaburi 33:1-22
33 Mupige vigelegele vya shangwe, kwa sababu ya Yehova, ninyi wenye haki.+
Ni jambo lenye kufaa kwa wanyoofu kumusifu yeye.
2 Mumushukuru Yehova kwa kinubi;
Mumuimbie sifa* kwa chombo cha kamba kumi (10).
3 Mumuimbie wimbo mupya;+
Mupige kamba kwa ufundi, pamoja na vigelegele vya shangwe.
4 Kwa maana neno la Yehova limenyooka,+
Na kila jambo lenye anafanya linategemeka.
5 Anapenda uadilifu* na haki.+
Dunia imejaa upendo mushikamanifu wa Yehova.+
6 Kwa neno la Yehova mbingu zilifanywa,+
Na kwa roho* ya kinywa chake kila kitu chenye kuwa katika mbingu kilifanywa.*
7 Anakusanya maji ya bahari kama vile ukuta wa maji;+
Anatia maji yenye mawimbi makubwa katika madepo.
8 Dunia yote imuogope Yehova.+
Wakaaji wa inchi yenye kuzaa wamuogope sana.
9 Kwa maana alisema, na ikakuwa vile;+
Aliamuru, na ikasimama imara.+
10 Yehova amevuruga mipango mibaya ya* mataifa;+
Amevunja mipango* ya vikundi vya watu.+
11 Lakini maamuzi ya Yehova yatasimama* milele;+
Mawazo ya moyo wake ni ya kizazi kwa kizazi.
12 Lenye furaha ni taifa lenye Mungu wake ni Yehova,+
Watu wenye amechagua kuwa mali yake mwenyewe.+
13 Yehova anaangalia chini akiwa mbinguni;
Anaona wana wote wa binadamu.+
14 Akiwa katika makao yake,
Anakazia macho wakaaji wa dunia.
15 Yeye ndiye anaumba mioyo ya wote;
Anachunguza kazi zao zote.+
16 Hakuna mufalme mwenye anaokolewa kupitia jeshi kubwa;+
Mutu mwenye nguvu haokolewe kupitia nguvu zake nyingi.+
17 Farasi ni tumaini la uongo la wokovu;*+
Nguvu zake nyingi hazihakikishe kuponyoka.
18 Angalia! Jicho la Yehova linalinda wale wenye kumuogopa,+
Wale wenye kungojea upendo wake mushikamanifu,
19 Ili awaokoe* katika kifo
Na kulinda uzima wao wakati wa njaa.+
20 Tunamungojea* Yehova.
Yeye ni musaidizi wetu na ngao yetu.+
21 Mioyo yetu inashangilia katika yeye,
Kwa maana tunategemea jina lake takatifu.+
22 Upendo wako mushikamanifu ukae juu yetu, Ee Yehova,+
Wakati tunaendelea kukungojea.+
Maelezo ya Chini
^ Ao “Mumupigie muziki.”
^ Angalia Maana ya Maneno.
^ Ao “jeshi lote la mbinguni lilifanywa.”
^ Ao “pumuzi.”
^ Ao “mawazo.”
^ Ao “shauri la.”
^ Ao “shauri la Yehova litasimama.”
^ Ao “la ushindi.”
^ Ao “aokoe nafsi yao.”
^ Ao “Nafsi yetu inamungojea.”