Zaburi 33:1-22
33 Mupige vigelegele vya shangwe, kwa sababu ya Yehova, ninyi wenye haki.+
Ni jambo lenye kufaa kwa wanyoofu kumusifu yeye.
2 Mumushukuru Yehova kwa kinubi;Mumuimbie sifa* kwa chombo cha kamba kumi (10).
3 Mumuimbie wimbo mupya;+Mupige kamba kwa ufundi, pamoja na vigelegele vya shangwe.
4 Kwa maana neno la Yehova limenyooka,+Na kila jambo lenye anafanya linategemeka.
5 Anapenda uadilifu* na haki.+
Dunia imejaa upendo mushikamanifu wa Yehova.+
6 Kwa neno la Yehova mbingu zilifanywa,+Na kwa roho* ya kinywa chake kila kitu chenye kuwa katika mbingu kilifanywa.*
7 Anakusanya maji ya bahari kama vile ukuta wa maji;+Anatia maji yenye mawimbi makubwa katika madepo.
8 Dunia yote imuogope Yehova.+
Wakaaji wa inchi yenye kuzaa wamuogope sana.
9 Kwa maana alisema, na ikakuwa vile;+Aliamuru, na ikasimama imara.+
10 Yehova amevuruga mipango mibaya ya* mataifa;+Amevunja mipango* ya vikundi vya watu.+
11 Lakini maamuzi ya Yehova yatasimama* milele;+Mawazo ya moyo wake ni ya kizazi kwa kizazi.
12 Lenye furaha ni taifa lenye Mungu wake ni Yehova,+Watu wenye amechagua kuwa mali yake mwenyewe.+
13 Yehova anaangalia chini akiwa mbinguni;Anaona wana wote wa binadamu.+
14 Akiwa katika makao yake,Anakazia macho wakaaji wa dunia.
15 Yeye ndiye anaumba mioyo ya wote;Anachunguza kazi zao zote.+
16 Hakuna mufalme mwenye anaokolewa kupitia jeshi kubwa;+Mutu mwenye nguvu haokolewe kupitia nguvu zake nyingi.+
17 Farasi ni tumaini la uongo la wokovu;*+Nguvu zake nyingi hazihakikishe kuponyoka.
18 Angalia! Jicho la Yehova linalinda wale wenye kumuogopa,+Wale wenye kungojea upendo wake mushikamanifu,
19 Ili awaokoe* katika kifoNa kulinda uzima wao wakati wa njaa.+
20 Tunamungojea* Yehova.
Yeye ni musaidizi wetu na ngao yetu.+
21 Mioyo yetu inashangilia katika yeye,Kwa maana tunategemea jina lake takatifu.+
22 Upendo wako mushikamanifu ukae juu yetu, Ee Yehova,+Wakati tunaendelea kukungojea.+

