Zaburi 95:1-11

  • Ibada ya kweli pamoja na utii

    • “Leo kama munasikiliza sauti yake” (7)

    • “Musifanye moyo wenu kuwa mugumu” (8)

    • “Hawataingia katika pumuziko langu” (11)

95  Mukuje, tumupigie Yehova vigelegele vya shangwe! Tumupigie vigelegele vya ushindi Mwamba wetu wa wokovu.+  2  Tuingie mbele yake* tukiwa na shukrani;+Tuimbe na kumupigia vigelegele vya ushindi.  3  Kwa maana Yehova ni Mungu mukubwa,Mufalme mukubwa juu ya miungu mingine yote.+  4  Sehemu za chini kabisa za dunia ziko katika mukono wake;Vichwa vya milima ni vyake.+  5  Bahari, yenye aliumba, ni yake,+Na mikono yake ilitengeneza inchi kavu.+  6  Mukuje, tuabudu na kuinama;Tupige magoti mbele ya Yehova Mutengenezaji wetu.+  7  Kwa maana yeye ni Mungu wetu,Na sisi tuko watu wa malisho yake,Kondoo wenye anatunza.*+ Leo kama munasikiliza sauti yake,+  8  Musifanye moyo wenu kuwa mugumu kama vile mulifanya kule Meriba,*+Kama katika siku ya Masa* katika jangwa,+  9  Wakati mababu zenu walinijaribu;+Wakanipima, hata kama walikuwa wameona kazi zangu.+ 10  Kwa miaka makumi ine (40) nilichukizwa na kizazi hicho, na nikasema: “Wao ni watu wenye kupotoka sikuzote katika mioyo yao;Hawajafikia kujua njia zangu.” 11  Kwa hiyo niliapa katika kasirani yangu: “Hawataingia katika pumuziko langu.”+

Maelezo ya Chini

Tnn., “mbele ya uso wake.”
Tnn., “wa mukono wake.”
Maana yake “Ugomvi.”
Maana yake “Kujaribu; Jaribu.”